Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha leo imeahirisha
usikillizaji wa ushahidi wa shahidi namba saba upande wa Jamhuri wa kesi
ya jinai namba 105 ya mwaka 2021 ya unyang'anyi wa kutumia silaha
inayomkabili aliyekuwa Mkuu wa wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro Lengai
Ole Sabaya na wenzake wawili kutokana na Mshtakiwa namba Moja Lengai Ole
Sabaya kutokufika mahakamani kutokana na sababu za kiafya.
Akiahirisha
shauri Hilo Hakimu Mkazi Mwandamizi Odira Amworo amesema shauri hilo
litaendelea kusikilizwa tena hapo kesho Agosti 05 asubuhi kwa kuendelea kusikiliza ushahidi wa
shahidi namba saba Mratibu Msaidizi wa Polisi ASP Gwakisa Minga ambaye
ni Mkuu wa Upelelezi wa makosa ya jinai wilaya ya Arusha.
Post A Comment: