Afisa Mwandamizi Mkuu Idara ya Matekelezo Mkoa wa NSSF Tanga Abubakari Mshangama akizungumza na waandishi wa habari wakati maonyesho ya wiki ya maziwa inayoendelea kwenye viwanja vya Tangamano Jijini Tanga

Meneja Kiongozi Mahusiano na Elimu kwa Umma, Bi. Lulu Mengele akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ushiriki wao kwenye maonyesho ya wiki ya maziwa
Meneja Kiongozi Mahusiano na Elimu kwa Umma, Bi. Lulu Mengele kushoto akieleza jambo kwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga Adam Malima wakati alipotembelea  Banda lao

Afisa Mwandamizi Mkuu Idara ya Matekelezo Mkoa wa NSSF Tanga Abubakari Mshangama kulia akimkabidhi vipeperushi mbalimbali Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji mara baada ya kutembela banda lao kushoto anayeshuhudia ni Meneja Kiongozi Mahusiano na Elimu kwa Umma, Bi. Lulu Mengele

NA OSCAR  ASSENGA,TANGA

SHIRIKA la Hifadhi za Jamii (NSSF) wameamua kushiriki maonyesho ya wiki ya maziwa inayoendelea kwenye viwanja vya Tangamano Jijini Tanga ili kutekeleza agizo la kuwafikia sekra isiyorasmi na wafanyabiashara wadogo wadogo.

Hayo yalisemwa na Afisa Mwandamizi Mkuu Idara ya Matekelezo Mkoa wa NSSF Tanga Abubakari Mshangama wakati akizungumza na waandishi wa habari ambapo alisema mpango huo wamepewa na serikali kuanzia mwaka 2018 kufikisha lengo la kuwafikia wananchi MIlioni 18.

Alisema katika kutekeleza agizo hilo na kupunguza umaskini kwa wananchi na kuongeza wigo wa uandikishaji Shirika hilo wameona washiriki kwenye maonyesho hayo lengo kuwahudumia  wafanyakazi ambao wapo kwenye sekta iliyorasmi na wananchi ambao hawapo kwenye sekta isiyorasmi ili kuwaonyesha mafao walionayo na utaratibu wa kujiunga na NSSF.

Alisema pia na taratibu za wanachama kupata mafao kwa sababu wamekuwa na mafao tofauti tofauti kama watu wengi ambao wapo kwenye sekta isiyorasmi na iliyorasmi wana fao la kukosa ajira lakini zamani ilikuwa fao la kujitoa.

“Fao la kukosa ajira zamani lilizoelewa fao la kujitoa lakini hivi sasa serikali imekuja na fao la kukosa ajira ambalo kwa watu ambao wana taaluma na elimu kidogo nzuri na wamechangia zaidi ya miezi 18 watalipwa asilimia 33.3 ya wastani wa mshahara wake wa mwisho lakini kama hatakuwa hajafikisha ile michango 18 watalipwa asilimia 50 ya michango yake”Alisema

Alisema lakini serikali haikuwatupa wale ambao hawana elimu au ujuzi zaidi hao watapewa asilimia 100 ya mafao yake ambapo mpango huo wa kuwa na sekta rasmi na isiyorasmi kupewa NSSF ni kuzidisha wigona kupunguza umaskini wa wananchi ikiwemo kutoa fursa zilizopo za hifadhi ya jamii kwa kujijengea maisha yao ya sasa na baadae.

Aidha pia alisema kuwa NSFF wanatoa mafao ya muda mfupi na muda mrefu ambapo muda mfupi ni mafao ya matibabu,uzazi,mazishi na ukosefu wa ajira huku akielezea mafao ya muda mrefu  ni pensheni ya urithi,pensheni ya uzee na pia kwa ajili ya mwanachama ambaye lakini alitakiwa kupata pensheni lakini akafariki basi familia yake itaendelea kunufaika.

Hata hivyo alisema kwa mkoa wa Tanga katika sekta isiyorasmi hivi sasa wameinuka kutokana na hamasa waliyoifanya ikiwemo kupitia maonyesho mbalimbali na semina wamepata mwamko watu wameanza kujiandikisha na kuanza kujua thamani ya hifadhi za jamii ni nini.

“Lakini hivi sasa tuna mpango wa kupitia kwenye vyuo vya Tanga na Taasisi zenye wajasiriamali wadogo na wakubwa ikiwemo kuwa na mabalozi wadogo wa NSSF ambao tukifundisha wakiwa wadogo basi baadae watasaidia kujua maana nzuri ya Hifadhi ya Jamii”Alisema

Share To:

TANGA RAHA BLOG

Post A Comment: