Jackline Kuwanda,Mpwapwa .Dodoma


Kamati ya  Wilaya ya ulinzi wa Wanawake  na Watoto Wilayani Mpwapwa Mkoani Dodoma imetembelea Gereza la Wanawake Wilayani humo na kuridhishwa na mwenendo wa huduma zinazotolewa kwa wanawake.


Baada ya kutembelea Gereza hilo leo  Mwenyekiti wa Kamati hiyo na Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya hiyo Paul Sweya  amesema wameridhishwa na Mazingira Mazuri katika Gereza na namna ambavyo wanawake wanahudumiwa hasa katika kupatiwa haki zao za Msingi kama wanawake.


"Tumeridhishwa na Mazingira kiukweli ni mazuri na hata mama anapokuwa hapa na Mtoto wake ameendelea kuhudumiwa vizuri,tumemkuta mahabusu mmoja na mfungwa mmoja ,huyu mfungwa aliyefungwa kama jamii yake ingemsaidia basi asingekuwa hapa ana watoto saba ambao wanaomtegemea na faini yake ilikuwa shilingi laki tatu tu,tunaona pia Gereza hili linawanawake wawili tu hii inamaana kuwa Elimu imetolewa zaidi" amesema Sweya 



Dodoma News Blog imezungumza na  Mrakibu Msaidizi wa Magereza na Mkuu wa Gereza sehemu ya  Wanawake Veronica Mwasalemba amesema mwanamke anapoingia gerezani husitiriwa vyema bila ya kumvunjiwa haki zake ambazo anastahili kuzipata kama Mwanamke .


"Mwanamke anapokuja hapa huwa tunamsitiri vizuri yeye pamoja na Mtoto kama yuko na Mtoto ,watu wengi  huwa wanaogopa sana wanaposikia gerezani hii  si sehemu  ya kuogopa mtu anapokuja hapa anajifunza mambo mengi na hata wakitoka hapa huko wanapokwenda huwa wamebadilika kutokana na Mafunzo ambayo wameyapata hapa" amesema Veronica 


Aidha Amesema anatamani kuona Gereza hilo linakuwa na Mazingira Mazuri zaidi lakini kutokana na Changamoto ya kutokuwepo kwa baadhi ya vitu ameiomba kamati hiyo Kusaidia Ili Gereza hilo la wanawake Ili Mazingira yawe mazuri zaidi 


"Unaona hapa kuna magodoro tunatamani vitanda vikawepo Ili na wao wawe katika Mazingira Mazuri  ,naimani kamati hii itasaidia "amesema Veronica 


Amesema wanawake wanaofungwa huacha pengo kuwa katika familia kwani ukiangalia yeye ndiye aliyebeba majukumu mazito ya kuhudumia familia lakini linapokuja suala la kufungwa husababisha hata watoto aliyowaacha kuishi bila ya kuwa na uangalizi mzuri.


"Unakuta mama kafungwa huku akiacha watoto saba ,unajiuliza hawa watoto huko nje wataishije na kama unavyojua mama yeye ndiye kila kitu katika familia ,na hata ikifika wakati wa kujitetea Mahakamani wengi wao huwa wanaogopa anaulizwa unakipi cha kuiambia mahakama anasema hana akishatoka ukimuuliza anasema alikuwa anaogopa ,huenda angeiambia mahakama kuwa anawatoto kadhaa wanaomtegemea kungekuwa na njia rahisi ya kumsaidia " amesema Veronica 


Kwa upande wa Hakimu Mkazi Wilayani humo Lusajo Mutua akizungumza na mtandao huu amesema jamii inaweza kukosa picha kwanini mwanamke amepata adhabu "mtu yuko Mahakamani anaulizwa kwanini mahakama isikupe adhabu hii ,yawezekana alipewa nafasi

ya kujitetea lakini kutokana na uelewa mdogo anashindwa kujitetea ,hapa ndipo watu wanakuja kuona kuwa mahakama haijafanya kazi yake lakini si Kweli ,sisi tunamjali mwanamke na tunatoa adhabu kwa mujibu wa Sheria " amesema Lusajo 


Mmoja wa wanawake ambaye anatumikia kifungo  Cha miezi minne gerezani  Neema Mazengo(si jina lake halisi )  mwenye watoto saba amesema  alifungwa kutokana na kupishana kauli na mama Mkwee  wake hali iliyopelekea kufungwa kwa miezi hiyo.


"Nilipishana kauli na mama Mkwee wangu hivyo niliamriwa kulipa faini ya shilingi laki tatu au kutumikia kufungo  Cha miezi minne , sababu ya kukosa pesa ilibinibidi kutumikia kufungo hicho ,baadàye mume wangu aliipata hiyo laki tatu alitaka kuja kunilipia nikamwambia alipie watoto ada shuleni Ili waendelee na masomo mimi nitumikie kifungo "amesema 


Shirika la Jukwaa la utu wa mtoto wilayani humo Children's Dignity Forum CDF kwa ufadhili wa Comic Relief kupitia mradi wa Haki ya Binti  wamewezesha  kikao cha robo mwaka cha kamati hiyo ambayo imekuwa na msaada mkubwa katika kuwasiadia wanawake na watoto pindi wanapokumbana na changamoto mbalimbali ikiwemo ya Vitendo vya ukatili dhidi yao.


Mwisho.

Share To:

msumbanews

Post A Comment: