Mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalengo, Maalim Seif Sharif Hamad leo amechukua fomu ya kugombea nafasi ya Urais visiwani Zanzibar kupitia chama hicho katika uchaguzi mkuu wa Viongozi utakaofanyika Oktoba mwaka huu.

Maalim Seif amekabidhiwa fomu hiyo leo na Katibu Mkuu wa ACT- Wazalendo, Ado Shaibu katika ofisi za Chama za Vuga Zanzibar.
Share To:

Post A Comment: