Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora imevishauri vyombo vya habari hususani runinga kuweka kipengele cha msomaji wa habari wa lugha ya alama wakati wa kurusha matangazo yao ili watu walemavu wa kusikia (Viziwi) nao waweze kuelewa taarifa zinazotolewa kuhusiana na ugonjwa na Ugonjwa unaosababishwa na virusi vya Corona.
Akizungumza na Wanahabari jijini Dodoma ,Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu amesema hali hiyo itatoa fursa kwa watazamaji wote wakiwemo wenye ulemavu kujua kinachoendelea huku pia akiipongeza wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii,Jinsia,wazee na watoto na watendaji wake kwa kutoa huduma stahiki kwa wanachi ambao tayari wemekwisha ambukizwa ugonjwa wa homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona (COVID-19).
Amesema jamii inapaswa kutokufanya mzaha na jambo hilo kwani janga hilo ni kubwa hivyo ni muhimu kuunga mkono jitihada za serikali kwa kufuata maelekezo sahihi ikwemo wale wote washukiwa wa maambukizi na wenye maambukizi kukaa karantini kwa muda ulipangwa ili kuzuia
maambukizi ya ndani kuongezeka.
Tume hiyo pia imeendelea kuwaomba wadau mbalimbali kuendela kujitokeza kuunga mkono jitihada za serikali katika mapambano dhidi ya maradhi hayo huku akitoa ushauri kwa serikali kuendelea kuchukua tahadhari
katika mipaka ili kuzuia kuingia kwa maambukizi mapya kutoka nje ya
nchi.
Tume hiyo pia imeipongeza Jumuiya ya asasi za kiraia AZAKI na wafanyabishara waliojitokeza kuunga mkono jitihada za serikali katika kupambana na ugonjwa huo.
Hatahivyo, Tume hiyo imeendelea kuipongeza serikali kwa juhudi kubwa inazofanya ya kupambana na mlipuko wa ugonjwa wa homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona (COVID-19) .
Tume hiyo pia imeendelea kuwaomba wadau mbalimbali kuendela kujitokeza kuunga mkono jitihada za serikali katika mapambano dhidi ya maradhi hayo huku akitoa ushauri kwa serikali kuendelea kuchukua tahadhari
katika mipaka ili kuzuia kuingia kwa maambukizi mapya kutoka nje ya
nchi.
Tume hiyo pia imeipongeza Jumuiya ya asasi za kiraia AZAKI na wafanyabishara waliojitokeza kuunga mkono jitihada za serikali katika kupambana na ugonjwa huo.
Hatahivyo, Tume hiyo imeendelea kuipongeza serikali kwa juhudi kubwa inazofanya ya kupambana na mlipuko wa ugonjwa wa homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona (COVID-19) .
Post A Comment: