Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuzindua safari za ndege za mizigo kwenda nje ya nchi ya Tanzania kwenye Uwanja wa Ndege wa Kilimanjaro
Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye (wa pili kulia) akishirikiana na wafanyakazi kupanga mizigo baada ya kuzindua ndege ya kusafirisha mizigo kwenda nje ya nchi kwenye Kiwanja cha Ndege cha Kilimanjaro
Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye akitoa maelekezo kwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa KADCO, Christopher Mukomu (wa pili
kulia) wakati akikagua chumba cha barafu cha kuhifadhia mizigo kilichopo kwenye Uwanja wa Ndege wa Kilimanjaro.
Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye akitoka ndani ya ndege baada ya kuzindua safari za ndege za mizigo kwenda nje ya Tanzania kwenye uwanja wa Ndege wa Kilimanjaro. Anayemfuata ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa KADCO, Christopher MukomuMkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira (kushoto) akizungumza na Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye (wa pili kulia) wakati wakisubiri kuwasili kwa ndege ya mizigo kutoka nje ya nchi kwenye Uwanja wa Ndege wa Kilimanjaro

KADCO yajenga chumba cha barafu chenye uwezo wa kubeba tani 110
Na Prisca Ulomi, WUUM, KIA
Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye amezindua safari za ndege za mizigo kwenye Uwanja wa Ndege wa Kilimanjaro (KIA) kwa ajili ya kuwawezesha wafanyabiashara, wakulima wa mazao, matunda na mboga mboga wa mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Tanga, Manyara na mikoa ya jirani kutumia usafiri huo kusafirisha mizigo yao kwenda nje ya nchi ya Tanzania.

Nditiye amesema kuwa uzinduzi wa safari za ndege za mizigo ni utekelezaji wa agizo la Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe wakati akizindua bodi ya Maendeleo ya Kiwanja cha Ndege cha Kilimanjaro (KADCO) mwaka jana mwezi Desemba.
“Niwapongeze sana KADCO kupitia Kaimu Mkurugenzi Mkuu wenu, Christopher Mukomu na kwa kushirikiana na Umoja wa Wakulima wa Mboga Mboga na Maua Tanzania (TAHA), mmeweza na kuhakikisha ujio wa ndege hii muhimu kwa ajili ya kusomba mizigo yetu hapa Tanzania, hilo kwangu mimi ni kitu kikubwa sana kwa sababu kwa miaka mingi hatukuwa na huduma ya mizigo kwa ndege kubwa kama hii, naipongeza sana Ethiopian Airline kwa utayari wao wa kushirikiana na Serikali na kuamua kuleta ndege yao ya mizigo kuja kubeba mizigo,” amesema Nditiye.
Pia, amekagua chumba cha barafu cha kuhifadhi mizigo inayosafirishwa na ndege kwenda nje ya nchi ya Tanzania na kujiridhisha kuwa chumba hicho cha kisasa kimejengwa, kinafanya kazi vizuri na kina uwezo wa kubeba tani 110 na kina hali nzuri na amewaomba wadau mbali mbali kutumia huduma hii kusafirisha mizigo yao badala ya kupitisha nchi za jirani.
Ameilekeza Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kukaa na wadau wa usafirishaji wa mizigo hiyo ili kuweza kutoa kibali cha muda mrefu cha wiki mbili au hata mwezi ili kuwawezesha wasafirishaji kutumia vizuri fursa hii na amewataka wazingatie sheria, taratibu na kanuni husika na siyo kutoa kibali tu, bali kutoa kibali cha kuhakikisha kuwa biashara hii inakuwa endelevu na kuzingatia usalama.
Nditiye ametoa maelekezo hayo baada ya Afisa Mtendaji Mkuu wa TAHA, Dkt. Jacquline Mkindi kuiomba Serikali kuweka mazingira wezeshi ya usafirishaji wa mizigo
kwenda masoko ya Ulaya ikiwa ni pamoja na ndege hizo kuja nchini kwa gharama nafuu kwa kupunguza tozo mbali mbali kwa ndege kila inapotua, kuongeza muda wa kibali cha ndege na kuwa na tozo tofauti baina ya ndege za mizigo na za abiria ili kuendelea kuzivutia ndege hizo na ndege nyingine za mizigo kuja KIA na kutumia fursa
hiyo kuiwezesha sekta binafsi na wakulima wa mboga mboga na maua kufanya biashara kwenye soko lolote duniani.

Uzinduzi wa safari za ndege za mizigo umehudhuriwa na Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga ambapo ameshuhudia wakulima wa mboga mboga na maua wa TAHAwakipakia mizigo ya bidhaa zao kwenda nje ya nchi ambapo Nditiye na Hasunga wameshiriki kupakia mizigo hiyo.
Naye Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira amesema kuwa Serikali inatambua mchango wa sekta binafsi na wakulima na lazima sekta binafsi ikuzwe a ilelewe kwa kupewa mashaerti nafuu ya kufanya biashara zao na itaendelea kuunganisha mnyororo wa thamani kwa kutumia viwanja vyake vya ndege na kununua ndege za mizigo kama ambavyo Serikali imefanya kwa kununua ndege za abiria.
Nditiye amefafanua kuwa kwa muda mrefu ndege ya KLM imekuwa ikitumia uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere uliopo Dar es Salaam kusafirisha mizigo kwenda nchi mbali mbali, Serikali imeanza kujenga chumba cha barafu cha kuhifadhi mizigo kwenye uwanja wa ndege wa Mbeya na katik mwaka wa fedha wa 2020/2021, Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano imetenga fedha ya kununua ndege ya kusafirisha mizigo
Share To:

Post A Comment: