Mbunge wa Isimani Mhe Wiliam Lukuvi 

Mbunge wa jimbo la Isimani Mhe Wiliam Lukuvi amesema zoezi la ufungaji TV katika vijiji vya jimbo hilo ni mpango wa serikali wa kuwezesha wananchi kupata taarifa mbali mbali .

Alisema serikali  toka mwaka jana ilianza kutoa dishi na ving'amuzi wakati kwa upande wake kama Mbunge alichangia TV ili wananchi waweze kufikiwa na mpango wa  elimu kwa umma  kwa kuwafanya wananchi hasa  wa vijijini wasio na uwezo wa kununua TV kila mmoja aweze kupata elimu hiyo . " Niliomba UCAF kama wabia wa serikali wakanipatia ving'amuzi na madish na mimi nikanunua  TV ili  kufunga kwenye maeneo  ambayo wananchi wameyaandaa na kuyawekea umeme  kwa gharama  zao kwenye vijiji vyote vya jimbo la Ismani"

Lengo ni kuwahabarisha wananchi  juu ya utekelezaji wa ilani  ya CCM ngazi ya  kitaifa, Kusikiliza hotuba  mbali mbali za  viongozi wa kitaifa, kuhabarika na kupata elimu ya matukio mbalimbali ya kitaifa na kimataifa" zihusuzo afya,kilimo, elimu,ufugaji,uvuvi,hali ya hewa, michezo alisema Lukuvi .

Pia alisema kuwa kwenye mkutano mkuu wa jimbo wananchi  uliofanyika mwaka jana wananchi waliomba zoezi la kusambaza TV hizo kuendelea kutolewa zaidi ili wote waweze kufuatilia vipindi vya elimu kwa umma kupitia TV .
Share To:

Francis Godwin Mzee wa matukiodaima

Post A Comment: