Serikali ya Yemen inayotambulika kimataifa na wapiganaji wanaotaka kujitenga upande wa kusini wametia saini makubaliano ya kugawana madaraka na kumaliza mapigano baina ya makundi hayo. 

Mwanamfalme wa Saudi Arabia Mohammed bin Salman alitangaza kufikiwa makubaliano hayo katika televisheni ya taifa jana, akisema ilikuwa hatua muhimu kufikisha mwisho vita vya miaka minne nchini Yemen. 

Makubaliano yanayoitwa ya Riyadh , yanakamilisha mwezi mmoja wa mazungumzo ya moja kwa moja ya amani kati ya serikali hiyo inayotambuliwa kimataifa, ikiongozwa na rais Abed Rabbo Mansour Hadi na wapiganaji wanaotaka kujitenga wakiungwa mkono na Umoja wa Falme za Kiarabu wanofahamika kama baraza la mpito la kusini mwa Yemen STC. 

Pande hizo mbili zimekuwa zikipigana licha ya kuungana dhidi ya majeshi ya wahouthi yanayoungwa mkono na Iran, ambayo yanashikilia mji mkuu Sanaa, pamoja na miji mingine mingi nchini Yemen.

-DW

Share To:

msumbanews

Post A Comment: