Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Waziri wa nchi,Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Mhe.Seleman Jafo ameziagiza Halmashauri Kote nchini kuwa na Mpango mkakati wa Kukutana na Taasisi za Dini angalau  Mara mbili  kwa Mwaka katika kujadili Mambo  mbalimbali kwani Taasisi hizo zimekuwa  na mchango mkubwa  kwa Taifa .
Waziri Jafo ameyasema hayo jijini Dodoma Sept.4,2019 wakati akifunga mkutano  wa  82 wa chama cha Madaktari wa kikristo Tanzania [TCMA] ambapo amesema miongoni mwa watu Muhimu katika Taifa lolote lile ni Madaktari na walimu ,hivyo viongozi wa Dini ni Walimu muhimu wanaosaidia kuelimisha jamii kuwa na maadili mema na Msingi Bora wa kuishi ikiwa ni Pamoja na kuepuka matendo maovu ya dawa za kulevya ,Wizi,Uvivu na Ugaidi.
Kutokatana na hilo Waziri Jafo ameagiza Halmashauri kote nchini Kufanya vikao na viongozi wa Dini angalau Mara mbili kwa Mwaka ili kuweza kujadili mambo muhimu ya Kujenga Taifa.
”Kati  ya watu muhimu katika Taifa hili na Duniani kote ni Madaktari  na Walimu,Ninyi viongozi wa Dini ni Walimu wazuri mnaobadilisha Tabia mbovu ya watu na kuwa na tabia nzuri .Kuna suala la utoaji wa huduma na Taasisi za kidini zimekuwa zinafanya vizuri,kwa hiyo tu mimi niagize halmashauri kote nchini kuwa na desturi ya kukutana na Taasisi za dini angalau mara mbili kwa mwaka katika kujadili changamoto mbalimbali kwani ninyi mmekuwa msaada kubwa kwa serikali”alisema.
Aidha,Waziri Jafo ameipongeza TCMA Kwa kuzindua  kampeni ya “Zijue Namba zako kwa Afya yako “kwani itakuwa chachu kubwa kuelimisha jamii kuhusu masuala ya Afya hususan Elimu ya Magonjwa yasiyoambukiza ambayo yameshamiri kutokana na ulaji usiozingatia Kanuni za bora za Afya hali inayopelekea kuwa na vitambi na Matatizo ya shinikizo la damu[Presha].
“Kati ya maeneo yenye  changamoto kubwa ni Magonjwa yasiyo ya kuambukiza watu wanakula Mapochopocho wanafikiri unene ni 
Share To:

msumbanews

Post A Comment: