WATU
wawili raia wa Afrika Kusini wamefariki katika ajali ya ndege
iliyotokea mapema asubuhi ya leo majira ya saa moja na nusu katika kata
ya Igigwa Wilayani Sikonge.
Watu
hao waliotambulika kwa majina ya D. Werner mwenye umri wa miaka hamsini
na nane 58 pamoja na Werner Fredrick Fronaman mwenye umri wa miaka 36
wote wanamme na raia wa Durbun Afrika ya kusini walikuwa kwenye ndege
yenye namba za usajili 19-ZU-TAF mali ya Afrika Kusini.
Akilezea
tukio hilo Mkuu wa Wilaya ya Sikonge Mhe. Peres Magiri alisema kuwa
amepokea kwa masikitiko makubwa tukio hilo na kusema kuwa watu hao
walikuwa katika ziara ya kuhamasisha wanafunzi barani Afrika kusomea
maswala ya Anga.
Kabla
ya ajali kutokea Ijumaa walitua kwa dharula katika uwanja wa ndege wa
Tabora wakitokea Entebe Uganda kuelekea Lilongwe Malawi ili kufika
Afrika ya kusini.
Jana asubuhi walipoanza safari, baada ya muda mchache walifanya mawasiliano na wataalamu wa uwanja wa ndege wa Tabora na kutoa taarifa kuwa injini ya ndege imezimika ghafla wakiwa angani hivyo wanafanya utaratibu wa kurudi Tabora.
Baada ya taarifa hizo hawakuweza kupatikana mpaka walipopata taarifa ya ajali hiyo na kufika wakakuta raia hao wameshafariki.
Jana asubuhi walipoanza safari, baada ya muda mchache walifanya mawasiliano na wataalamu wa uwanja wa ndege wa Tabora na kutoa taarifa kuwa injini ya ndege imezimika ghafla wakiwa angani hivyo wanafanya utaratibu wa kurudi Tabora.
Baada ya taarifa hizo hawakuweza kupatikana mpaka walipopata taarifa ya ajali hiyo na kufika wakakuta raia hao wameshafariki.
Post A Comment: