Baadhi ya viongozi wapya wa jeshi-usu la uhifadhi wakila kiapo cha utii katika hafla ya kutunuku vyeo vipya kwa watendaji wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania. Halfa hiyo imefanyika katika Kituo cha Mafunzo ya jeshi-usu, Mlele mkoani Katavi.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania Jenerali Mstaafu Geogre Marwa Waitara akimvisha cheo cha Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa mawasilino TANAPA Pascal Shelutete katika hafla ya uvishaji vyeo kwa Maafisa wa TANAPA.
Kamishna wa Uhifadhi wa TANAPA Dk. Allan Kijazi akishuhudia uvishwaji wa cheo kwa Naibu Kamishna wa Uhifadhi na Maendeleo wa TANAPA Wiliam Mwakilema unaofanywa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania TANAPA Jenerali Mstaafu George Waitara
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania TANAPA Jenerali Mstaafu Geogre Marwa Waitara akimvisha cheo cha Kamishna Mwandamizi Kanda ya Kusini Dkt. Christopher Timbuka .
Kamishna Msaidizi Huduma za Shirika Kanda ya Kusini Rukia Mkakile akiwa kwenye ukakamavu huku akipiga saluti kama heshima baada ya kuvishwa cheo hicho na Mwenyekiti wa Bodiya Wadhamini ya Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania TANAPA Jenerali Mstaafu Geogre (Waitara hayupo pichani)
Picha ya pamoja ya Wajumbe wa Bodi ya Wadhamini ya TANAPA na Makamishna Wandamizi mara baada ya kuvikwa vyeo hivyo, Halfa hiyoimefanyika katika kituo cha mafunzo ya jeshi-usu Mlele mkoani Katavi.
Baadhi ya watendaji wapya wakimsikiliza Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania TANAPA Jenerali Mstaafu Geogre Marwa Waitara katika hafla ya kutunuku vyeo vipya kwa watendaji wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania TANAPA
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya TANAPA Generali Mstaafu Geogre Marwa Waitara akikagua gwaride la wahitimu wa mafunzo ya jeshi usu.
Post A Comment: