Na Ferdinand Shayo ,Arusha.
Spika wa Bunge la Afrika Mashariki Dr.Martin Ngoga amezitaka nchi mwanachama wa jumuiya hiyo kutekeleza  mkataba wa Malabo unaozitaka nchi hizo kutenga asilimia 10% ya bajeti zao na kuielekeza kwenye kilimo ili kuhakikisha upatikanaji wa chakula na kukuza uchumi kupitia kilimo.
Akizungumza katika Mkutano Maalumu kati ya Bunge hilo na Wakulima wadogo pamoja na Asasi za kiraia zinazojihusisha na masuala ya kilimo uliofanyika jijini Arusha ,Spika huyo amesema kuwa nchi nyingi za EAC zimekua zikisua sua katika kutekeleza mkataba huo hivyo wanapaswa kuutekeleza.
Aidha amesema kuwa iwapo mkataba huo utekelezaji  utasaidia kutokomeza tatizo la udumavu na matatizo ya lishe miongoni mwa watoto ambao ndio kizazi kinachotegemewa kwa maendeleo ya Afrika Mashariki miaka ijayo.
Mkulima mdogo kutoka nchini Tanzania Sophia Boke amesema kuwa changamoto iliyoko kwa sasa wakulima wanatumia majembe ya mikono na wanakabiliwa na ukosefu wa mbegu bora na pembejeo kwa ujumla suala ambalo linarudisha nyuma maendeleo ya kilimo.
Mwanachama wa Shirika lisilokua la kiserikali la ESAFF ,Abdul Gea amesema kuwa fursa ya kuhudhuria katika bunge la EALA inatoa nafasi kwao kufikisha madai ya msingi ya wakulima na kuhakikisha mkataba wa Malabo unatekelezwa ili kuinua sekta ya kilimo.
Share To:

Post A Comment: