NA HERI SHAABAN,DODOMA
MWENYEKITI wa Taasisi ya Utalii 255 Mbunge wa Mkoa wa kaskazini Unguja Angelina Malembeka ,amewataka Watanzania kuweka mazoea ya kutembelea hifadhi mbalimbali za Mbunga za Utalii, zilizopo Tanzania ili waweze kujifunza Utalii wa ndani.
Mbunge Malembeka aliyasema hayo Bungeni Dodoma mwishoni mwa wiki , wakati akizungumza na waandishi wa habari mara baada kupokea wageni wake ,Wahamasishaji wa Kundi la Utalii 255 kutoka Tanzania Bara walikaribishwa kundi la utalii walishiriki kusikiliza kikao cha maswali na majibu Bungeni Dodoma.
Alisema ziara ya Wahamasishaji wa Utalii wa 255 Kutoka Tanzania Bara na Visiwani Zanzibar wapo katika ziara ya siku tatu ,wameanza kutembelea Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada hapo ziara inaelekea kutembelea Mbuga ya Hifadhi ya Taifa ya Tarangile Mkoa wa Mnyara.
"Hii ni sehemu ya kampeni ya kutangaza Utalii wa ndani ,kundi la Utalii 255 linawataka Watanzania kuweka mazoea ya kutembelea hifadhi za Taifa kuangalia mambo mbalimbali ikiwemo wanyama kama sehemu ya kujifunza"alisema Malembeka
Alisema Utalii 255 ilianzishwa hivi karibuni,ikiwa na lengo la kuwahamasisha na kuwakumbusha Watanzania kuweza kujiwekea utaratibu wa kutembelea Hifadhi na Vivutio vya Utalii vilivyopo Nchini, Ziara hii imewashirikishaka Vijana kutoka Tanzania Bara na Visiwani Zanzibar.
Alisema kampeni hiyo ya uhamasishaji utalii inatembelea hifadhi mbalimbali za Taifa kujifunza kisha kwenda kutangaza elimu hiyo kwa jamii wajue umuhimu wa kutembelea utalii wa ndani
Mwisho
Post A Comment: