Rais John Magufuli amesema anatamani kuendelea kuwepo kwa vyama vingi vya upinzani ili kuongeza ushindani, huku CCM ikiendelee kupata ushindi

Kauli hiyo ya Rais Magufuli ilitofautiana na Mkuu wake wa Mbeya, Albert Chalamila aliyetaka kibaki chama kimoja tu.

"Tunaweza kuwa na ‘Magufuli Ruling Party’ na mambo yakaenda vizuri kabisa," alisema RC Chalamila.

Leo katika ziara yake mkoani Mbeya Rais Magufuli ataweka jiwe la Msingi la ujenzi wa nyumba za walimu, mabwenu na maabara katika Chuo cha Ualimu Mpuguso na kuzungumza na wananchi wa Tukuyu.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: