Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Dkt Anna Mghwira akiwa ameongozana na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa Kilimanjaro wakitembelea maeneo yaliyoathirika na mvua iliyonyesha juzi ikiambatana na upepo.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Dkt Anna Mghwira akizungumza na mmoja wa maafisa wa Magereza waliokuwa katika uismamizi wa wafungwa wakati wa kukata miti mikubwa iliyofunga barabara baada ya kuanguka.
Moja ya miti mikubwa iliyoanguka katika ya barabara ukiwa umekatwa.
Kukatika kwa miti hiyo kulikuwa ni fursa kwa watu wengine waliojitokeza kuokota kuni.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Dkt Anna Mghwira akitizama mafundi wa shirika la umeme Tanesco wakati wakijaribu kurejesha miundo mbinu ya umeme iliyoharibika kufuatia mvua iliyoambatana na upepo.
Mafundi wa TANESCO wakijaribu kurejesha nyaya zilizokatika .
Sehemu ya nyaya zilizokatika kufuatia mvua hiyo.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro akiwa ameongozana na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wakitembelea Kiwanda cha kuzalisha vifaranga vya kuku ambacho kuta zake zilianguka pamoja na mti mkubwa kukatika.
Mti ulikuwa jirani kabisa na jengo lililokuwa na mashine za kuangulia vifaranga na kuharibu mashine mbili pamoja na kuahribu mayai zaidi ya 15,000.
Mafundi wakijaribu kuondoa sehemu ya mti ulioangukia jengo hilo.
Sehemu ya mashine hizo.
Mayai yakiwa kwenye mashine tayari kwa ajili ya kuanguliwa.
Vifaranga vya kuku vikiwa katika mashine baada ya kuanguliwa.
Kuku wakubwa wakiwa katika kiwanda hicho kwa ajili ya mayai.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Dkt Anna Mghwira akitizama moja ya nyumba ya mwalimu katika shule ya sekondari ya Old Moshi ambaye paa la nyumba hiyo liliezuliwa kutokana na upepo.
Nyumba nyingine katika shule ya sekondari ya Old Moshi ikiwa imeezuliwa na upepo.
Moja ya miti iliyoanguka katika shule ya sekondari ya Old Moshi ,mti huu uliangukia bweni la wananfunzi bahati nzuri haukuweza kusababisha madhara. 
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Dkt Annag Mghwira akitoa pole kwa wanafunzi wa shule ya sekondari ya Old Moshi alipowatembelea kuwajulia hali baada ya mvua iliyoaambatana na upepo kuharibu baadhi ya miundo mbinu zikwemo nyumba za walimu.
Baadhi ya wanafunzi katika shule ya sekondari ya Old Moshi wakimsikiliza Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Dkt Anna Mghwira (hayupo pichani).

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii,Kanda ya Kaskazini.
Share To:

Post A Comment: