Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Mafunzo kwa Njia ya Mtandao (TaGLA), Charles Senkondo akielezea majukumu ya ofisi yake kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Mary Mwanjelwa alipofanya ziara ya kikazi katika ofisi hiyo jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuhimiza uwajibikaji.

Dkt. Mary na Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Mafunzo kwa Njia ya Mtandao (TaGLA), Charles Senkondo   wakishuhudia teknolojia ya mawasiliano kwa njia ya video kwa kuunganishwa na Chuo cha Utumishi wa Umma Nairobi, Kenya, alipofanya ziara ya kikazi katika ofisi hiyo jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuhimiza uwajibikaji.

Dkt. Mary Mwanjelwa , Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Mafunzo kwa Njia ya Mtandao (TaGLA), Charles Senkondo na watumishi wa TaGLA wakishuhudia teknolojia ya mawasiliano kwa njia ya video kwa kuunganishwa na Chuo cha Utumishi wa Umma Nairobi, Kenya.

Meneja TEHAMA wa Wakala wa Mafunzo kwa Njia ya Mtandao (TaGLA), Emmanuel Tessua akitoa ufafanuzi jinsi teknolojia inavyofanya kazi katika wakala huo kwa Naibu Wazir Dkt. Mary Mwanjelwa, alipofanya ziara ya kikazi katika ofisi hiyo jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuhimiza uwajibikaji.

Naibu Waziri, Dkt. Mary Mwanjelwa akipokea zawadi kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Mafunzo kwa Njia ya Mtandao (TaGLA), Charles Senkondo alipofanya ziara ya kikazi katika ofisi hiyo jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuhimiza uwajibikaji.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: