Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii.

Baadhi ya walimu wa shule za sekondari nchini ambao wameshiriki katika maonesho ya Young Scientists Tanzania yanayoendelea katika ukumbi wa Kimataifa wa mikutano wa Mwalimu Nyerere, wamekubali kuwa wao ndio wamekuwa wazito kubadilika na mazingira ya teknolojia ya ufundishaji katika karne hii ya 21.

Hayo yamesemwa na Mtalaamu wa Mawasiliano kutoka Dot Tanzania , Ndimbumi Mwisongole alipokuwa akitoa majumuisho kwa walimu hao ambao wameshiriki mafunzo maalumu yaliyaondaliwa na Mfuko wa Ufadhili na Kuendeleza Ubunifu na Maendeleo ya watu (HDIF).

“tumeweza kuzungumza na walimu Zaidi ya 50 ambao wameshiriki warsha hii na wote wamekiri kuwa wao ndio wamekuwa wazito kubadilika kutokana na Teknolojia inavyokwenda katika sekta ya elimu.

Mwisngole amesema kuwa umefika wakati wa Walimu kuanza kubadilika na kutumia mtandao kwa ajili ya kupata matirio ya kufundishia ambayo wameyapata popote wanaposafiri kwenda kufundisha” amesema Mwisongole.Mwisongole ametoa wito kwa walimu wote kote nchini kuanza kutumia mtandao kwa ajili kujipatia matio ya kufundushia nakuacha kufikiaria kutembea na mavitabu mengi wakati wanaweza kutimia mtandao kuhifadhi kazi zao.

Kwa upande wake Mtengenezajai wa Vikaragosi vya Ubongo Kids Nisha Ligon amesema kuwa programu yake imekuwa kivutio kikubwa sana kwa watoto na kusaidia kuongeza uelewa mashuileni .
Kiongozi Mkuu wa Shirika la Ufadhili wa Ubunifu kwa Maendeleo ya Binadamu(HDIF), David Mc. Ginty akizungumza na Walimu wanaoshiriki Maonesho ya Wanasayansi Chipukizi ambapo tasisi yake ya HDIF ilipata Wasaa wa kutoa Mhadhara juu ya Ubunifu kwa walimu wa Masomo ya Sayansi Jijini Dar es Salaam.
Meneja Mawasilinao wa Taasisi Digital Opportunity Trust (Dot Tanzania), Ndimbumi Mwesongole akizungumza na Walimu kuhusu progarmu ya elimu kupitia mtandao kwa walimu kujipatia mtandao.
Mwanzilishi na Muongozaji wa Programu ya Vikaragosi vya kufundishia vya Ubongo Kids , Nisha Ligon akizungumza kuhusu uzoefu wake wa kufundisha kwa kutumia Vikaragosi kwa wanafunzi wa shule za msingi na Sekondari .
Mmoja wa Walimu walioshiriki katika Warsha hiyo iliyoandaliwa na HDIF akichangia mada wakati wa mafunzo.
Sehemu ya Walimu walioshiriki katika Mafunzo hayo wakifatilia kwa makini mafunzo yanayotolewa na wataalamu.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: