Joseph Ngilisho ,Arusha
Wataalamu wa manunuzi ya Umma nchini wametakiwa kuzingatia  weredi  katika utendaji  wao wa kazi na kuepukana na  vitendo vya ubadhilifu ,rushwa na matumizi mabaya  ya fedha za umma  jambo litakalosaidia kudhibiti matumizi mabaya ya fedha na  kusaidia   fedha hizo kutumika katika maendeleo mapana zaidi ya Taifa.
Akiongea kwa niaba ya Rais John Magufuli,wakati alipokuwa akifungua mkutano wa siku tatu wa wataalamu na wabobezi wa manunuzi ya umma(IPPC) kutoka nchini 46 duniani unaofanyika jijini Arusha,nchini Tanzania,waziri wa fedha na mipango dkt.Philp Mpango amesema mkutano huo  unalenga kujadiliana namna ya kudhibiti matumizi mabaya ya fedha za umma kupitia taknolojia mpya ya manunuzi .
‘’Ununuzi wa umma ndio sehemu kubwa ambapo fedha za bajeti zinapita  hivyo ukifanyika vibaya maana yake serikali inapata hasara ndio maana tunasisitiza weredi wa wataalamu wa manunuzi kwa sababu kuna mamunuzi hewa na miradi hewa ’amesema dkt Mpango
Aidha amesema asilimia 70 ya fedha za matumizi ya kawaida zinapitia ununuzi wa umma na asilimia 100 ya bajeti  ya fedha zote za maendeleo zinapitia manunuzi ya umma ,hivyo bajeti zote katika maeneo hayo mawili zikitumika vibaya lazima serikali iumie.
Amesema wataalamu wa manunuzi ya Umma wakitumia vizuri taaluma yao itasaidia maeneo mengine ya sera katika kukuza viwanda na kuinua sekta binafsi hivyo ununuzi utumike vizuri ili kusaidia kuinua nchi za afrika ikiwemo Tanzania kuendana  na teknolojia iliyopo.

Awali Mwenyekiti wa bodi ya manunuzi ya umma nchini,dkt Hellen Bandiho  amesema taasisi yao imeanza kuchukua hatua kwa wataalamu wake wasiozingatia weredi na maadili katika kazi zao na kuwataka waajiri kuhakikisha wanachukua wataalamu  wa manunuzi ya umma wenye usajiri wa  bodi yao.
‘’Wataalamu wa manunuzi ya umma wasio na usajiri ambalo wameajiriwa ama kufanya kazi zao bila usajiri ni makosa kwao na kwa mwajiri aliyewaajiri na hatua kali zitachukuliwa’’Amesema dkt Bandiho
Alivitaka vyombo vya dola kama polisi,takukuru na mahakama kushirikiana katika kuwaibuka na kuwachukulia hatua watu hao ambao wamekuwa wakiipaka matope bodi hiyo kwa kuendesha shughuli zako kinyume cha sheria.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: