Na Mwandishi Wetu
01/07/2018
MTENDAJI MKUU WAKALA WA MAJENGO TANZANIA(TBA) Arch; ELIUS ASANGALWISYE MWAKALINGA AONYESHA UWEZO MKUBWA KATIKA KUSIMAMIA UBORA WA MIRADI NA KUOKOA FEDHA ZA UMMA.
Nimepitia taarifa ya maendeleo ya Mradi mkubwa wa nyumba za Makazi Ujulikanao kama MRADI WA NYUMBA ZA MAKAZI MAGOMENI KOTA,
Kilichonifurahisha ni namna ambavyo Mtendaji mkuu wa Arch. Mwakalinga alivyochukua hatua mbalimbali katika kuokoa fedha za Umma na kuhakikisha Mradi unatekelezwa kwa Ubora [pamoja na changamoto mbalimba wanazokutana nazo wakati wa Utekelezaji wa Mradi,
Katika Taarifa hiyo fupi ya Utekelezaji wa Mradi huo unaotekelezwa kwa pamoja na Wizara ya Ujenzi Uchukuzi, na Mawasiliano, Wizara ya fedha na Wakala wa majengo Tanzania TBA Kila mmoja akiwa na majukumu yake maalumu kwenye Mradi huo.
.
Utekelezaji wa Mradi huo ulianza kwa wataalamu wa TBA kufanya Ubunifu wa majengo na wale wa BICO-UDSM Kufanya uchunguzi wa udongo ili kubaini uwezo(bearing capacity) wa kuhimili uzito wa majengo unaotarajiwa kujengwa, wakati huo huo wakala wa majengo aliendelea kufuatilia vibali kutoka mamlaka mbalimbali zikiwemo NEMC, Manispaa, AQRB na ERB Haya yote yalifanyika ili kukidhi mahitaji ya kisheria kwenye sekta ya ujenzi.
Mradi huu una jumla ya vitalu vitano (5Blocks) vitalu vinne vina ghorofa nane na mija ina ghorofa tisa na pia kitaru kimoja kinabeba kaya 126 ni mradi mkubwa na wakisasa kwa hapa kwetu nchini. Mradi mzima unauwezo wa kubeba Kaya 656 maana vitalu vinne vinabeba kaya 512 kitalu kimoja kinauwezo wa kubeba kaya 144,.
Hadi sasa mradi umeweza kukamilisha ujenzi wa msingi kwa Asilimia mia moja ( 100%) na Asilimia 35% kwa kazi ya juu ya msingi, Kama kawaida yake Mtendaji mkuu wa wakala wa majengo Tanzania Arch , Mwakalinga amekuwa akifanya majaribio ya uchunguzi wa wa zana mbalimbali kwenye maabara mbalimbali kati kuhakikisha vifaa vya ujenzi kwenye mradi huo ni zenye Ubora unaohitajika kwa mujibu wa maelekezo ya Kitaalamu, Vifaa vinavyochunguzwa mara kwa mara ni kama vile Mchanga, Kokoto, nondo na zege na maabara zilizotumika ni kama vile Chuo kikuu cha Dar es Salaam, BICO, na DIT,
Tathimini ya gharama za mradi zilizotumika mpaka sasa kulingana na tathimini iliyofanywa na wakadiriaji majengo Mradi umeweza kugharimu kiasa Cha 14,497.144,106,.65 (Shilingi za kitanzania) na Makisio ya gharama za kumaliza mradi (FRAME) Mradi una jumla ya bock tano zenye jumla ya floor arobaini na moja mpaka sasa kati ya hizo flppr kumi na mbili zimekamilika kwa hatua ya frame, Makisio kwa floor moja ni shilingi 438,611,875,00 hivyo basi makisio ya gharama ili kuweza kumaliza floor zilizobaki (floor 29) ni 12,719,744,375.00( Shilingi bilioni kumi na mbili milioni mia saba kumi na tisa laki saba arobaini na nne mia tatu sabini na tano)
HAPA NDIPO NINAPO MPONGEZA ARCH. ELIUS ASANGALWISYE MWAKALINGA
.
Mtambo wa Kisasa wa Kuzalisha Zege umeweza kudhalisha kiasi cha mita za ujazo 5799.800 kwa miradi mbalimbali ya mkoa wa DSM kama vile magomeni kota, Ukonga, TPA, Bandari, Osha na Ujenzi wa nyumba ya Rais mstaafu Jakaya Mrisho kikwete unaofanyika Kawe
Maamuzi ya kununua Mtambo wa kuzalisha zege yaliyofanywa na wakala wa majengo Tanzania umeleta faida nyingi sana na kuokoa fedha nyingi pia moja ya faida hizo ni (a) Kupungua kwa gharama za uzalishaji wa zege
(b) Kuokoa muda wa utendaji kazi
(c)Ubora wa zege kwa kuwa TBA wanazalisha wenyewe
(d) Matumizi sahihi ya malighafi kama kokoto, mchanga,na simenti.
CHANGAMOTO NA UTATUZI WAKE.
.
Arch E. A Mwakalinga akiwaongoza wataalamu wenzake katika mradi huu alikumbana na changamoto mbalimbali ikiwemo kupanda kwa bei ya vifaa vya ujenzi mfano, bei ya awali ya nondo ilikuwa shilingi milioni moja laki sita na ishilini mapa milioni moja na laki nane na bei ya sasa ni shilingi milioni mbili laki mbili na nusu kwa tani,
Lakini kwa weledi mkubwa Mtendaji mkuu wa wakala wa majengo Arch. Mwakalinga aliweza kutatua changamoto hii kwa kupata wazabuni ambao wana supply vifaa kwa bei nafuu na maamuzi yenye busara kwa kununua mtambo na magari ambayo yatapunguza kupata kwa gharama za Mradi.
KUOKOA FEDHA ZA UMMA.
.
Kwa kutumia wakala wa majengo Tanzania chini wa uongozo wa kizalendo wa Arch . Mwakalinga Serikali imeweza kuokoa mabilioni ya fedha Mfano wa miradi hiyo ni kama ifuatayo,
Miradi waiyookoa fedha za umma ni
.
1. Ujezi wa Hostels chuo kikuu - Wakala wa majengo Tanzania TBA mejenga kwa 10b against zaidi ya 80b za Wakandarasi wapigaji
2.Ujenzi wa ihungo Sec wakala wa majengo Tanzania TBA walijenga kwa 13b against 40b za wapigaji
3.Ujenzi wa Hospital Geita Wakala wa majengo Tanzania waliweza kujenga na kukamilisha kwa 17b against 75b ya private contractors (Wapigaji)
4. Ujenzi wa Hospital Chato Wakala wa majengo Tanzania walijenga kwa 15b against 65b private( Wapigaji)
5. Ujenzi wa Hospital Simiyu Wakala wa majengo Tanzania waliweza kujenga na kukamilisha kwa 12b against 36b private(Wapigaji)
Ukipiga hesabu utaona wameokoa kiasi kikubwa cha fedha ya serikali ambayo imeingia kuwahudumia wananchi kwenye miradi ya maendeleo.Kwanini mimi David Maphone nisipoteze muda wangu kumpongeza Mzalendo wa aina hii ya Arch Mwakalinga
Jambo kama hili haliwezei kuwafurahisha wezi waliokuwa wakitaka Wakala wa Majengo Tanzania TBA aendelee kukodi mitambo na magari ili kuongeza gharama za Mradi na wapo hata waheshimiwa wabunge wanatumika kufanya hujuma hizi, Mtendaji mkuu wa wakala wa majengo amemuunga mkono Rais Magufuli kwa kununua Mtambo sio kukodi kwa sababu hata Mhe Rais alipinga wazo la wabunge kukodi Ndege na badala yake aliamua kununua kabisa ili kukwepa gharama na kutuleteaa maendeleo ya uhakika.
.
Katika kuunga mkono TBA maendeleo ya mradi wa Magomeni kota na Taarifa ya TBA Mbunifu Majengo anayeheshimika sana kwa uwezo wa kiutendaji kupitia mchangu wake kwenye moja ya Group za WhatsApp
Arch. Humphrey Zachary Killo amesema ''Mradi huu ni muhimu kwa wakazi wa DSM na maendeleo yake ni makubwa tuwaunge mkono'
KWA UDANI ZAIDI USIKOSE KUSOMA RIPOTI YA UTEKELEZAJI WA MRADI ITAFUATA
Post A Comment: