Baaada ya tetesi nyingi kusambaa kwamba mwanamuziki Diamond Platinumz inawezekana amerudiana na mama mzazi wa watoto wake Zari the bossy ambae kwa sasa yuko Afrika ya Kusini, sasa imethibitika baada ya kusambaa kwa picha ikimuonyesha msanii huyo akiwa na watoto wake.

Pamoja na kwamba mara ya kwanza alikuwa akisema amekuwa akienda kuwaona watoto wake afrika ya kusini lakini hakukuwahi kuwa na picha iliyowahi kuthibitisha  hilo mpaka jana walipotoa picha hiyo kwa mara ya kwanza kwa takribani miezi minne tangu walipokuwa wamegombana
Share To:

msumbanews

Post A Comment: