Serikali ya awamu ya tano kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu imesema itafanya zoezi la ukaguzi nchini nzima katika sehemu za kazi ikiwemo kampuni ya ACACIA ili iweze kuwabaini waajiri ambao hawazingatii vigezo na masharti wanayopaswa kuwafanyia wafanyakazi wao.

Kauli hiyo imetolewa leo Mei 07, 2018 na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Walemavu, Anthony Mavunde Bungeni Jijini Dodoma kwenye kikao cha 23 mkutano wa 11 wa Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wakati akijibu la Mbunge wa viti maalum Jocye B. Sokombi aliyetaka kusikia kauli ya serikali juu ya tatizo la wafanyakazi wa mgodi wa Nyamongo kutolipwa mshahara wala posho pindi wafanyapo kazi zao.

"Mgodi wa dhahabu wa Nyamongo unamilikiwa na kampuni ya ACACIA na kwenye mgodi huo kuna makundi mawili ya wafanyakazi ambapo moja ni wale walioajiriwa na ACACIA na pili wafanyakazi waliajiriwa na makampuni yanayopewa kazi na ACACIA 'sub contractors'. Hivyo kwa wafanyakazi walioajiriwa na ACACIA wao hawalipwi posho bali hulipwa mshahara kwa mwezi", amesema Mavunde.

Pamoja na hayo, Mavunde ameendelea kwa kusema "makampuni mengine huwa wanalipwa mishahara kutokana na aina ya mikataba ya ajira na asili ya kazi anayoifanya mfanyakazi kwa kuzingatia sheria. Ofisi yangu kupitia idara ya kazi itaendelea kufanya kaguzi za kazi katika sehemu za kazi mbalimbali nchini ikiwepo kampuni ya ACACIA kwa lengo la kuwatambua waajiri ambao hawazin gatii matakwa ya sheria za kazi yanayotakiwa".

Kwa upande mwingine, Naibu Waziri Antony Mavunde amesema idara ya kazi imekuwa na taratibu za kufanya ukaguzi katika makampuni yote kwa lengo la kujua changamoto mbalimbali zinazojitokeza kwa wafanyakazi.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: