Mwandishi Wetu,Arusha

Mkuu wa mkoa Arusha,Mrisho Gambo ameagiza halmashauri zote za mkoa Arusha kupanda miti 1.5 milioni kwa mwaka ili kutunza mazingira.

Gambo alitoa hutuba hiyo kwenye maadhimisho ya upandaji miti mkoa Arusha ambayo yalifanyika kijiji cha Selela wilaya ya Monduli. 

Katika hutuba ya Gambo ambayo ilisomwa na Mkuu wa Wilaya ya Karatu,Theresia Muhonga alisema ili kufanikisha hilo,kila halmashauri inapaswa kutenga fedha kila mwaka.

"Tengeni fedha kila mwaka kusaidia kupanda miti na kuihifadhi" alisema

Mkuu huyo wa mkoa alizitaka halmashauri kushirikiana na wadau mbali mbali ili kufanikisha hilo zikiwepo sekta binafsi.

Awali Meneja Masoko wa kampuni ya Mobisol,David Ngwale ambao walikuwa sehemu ya wadhamini wa zoezi hilo,alisema suala la utunzwaji mazingira ni la watanzania wote.

Alisema kampuni yao ambayo huzalisha umeme wa jua itaendelea kusambaza huduma huyo hasa maeneo ya vijijini ili kuzuia uharibifu wa mazingira katika kupata nishati ya umeme.
  
Mkurugenzi wa halmashauri ya Monduli,Stivin Ulaya alisema wilaya hiyo kwa kushirikiana na wadau ikiwepo Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro imejopanga kukabiliana na uharibifu wa mazingira.

"Tumekuwa na miradi ya kupanda miti,kuhimiza majiko sanifu na tunashukuru wadau kama Mamlaka ya hifadhi Ngorongoro kusaidia" alisema.

Meneja wa malisho ya wanyama katika mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro, Hillal Mushi alisema Mamlaka hiyo itaendelea kushirikiana na serikali  misitu na kulinda vyanzo vya maji.

Alisema NCAA pia imekuwa na miradi ya kusambaza miti bure vijijini ili kuhakikisha mazingira yanatunzwa kwa manufaa ya sasa na vizazi vijavyo.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: