MWANAMKE Fatuma ambaye video yake ilisambaa katika mitandao ya kijamii ikimwonyesha akidai kwamba amekuwa akimtafuta baba yake tangu akiwa darasa la sita, amemwomba radhi Waziri Mstaafu, Edward Lowassa kwa kumdhalilisha.

Fatuma amesema hakutegemea kama ingekuwa hivyo ilivyotokea na kwamba, jambo hilo linamnyima amani. Pia ameiomba radhi familia ya mwanasiasa huyo na Watanzania kwa ujumla kutokana na kitendo hicho.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: