Timu ya Tottenham hapo jana imefanikiwa kuchomoka na sare ya mabao 2 – 2 baada ya kubanwa mbavu ikiwa ugenini dhidi ya Juventus michuano ya klabu bingwa barani Ulaya.
Mchezaji hatari wa Juventus,Gonzalo Higuain aliiyandikia timu yake mabao mawili katika dakika 45 za kipindi cha kwanza kabla Spurs kuanza kurudisha kupitia kwa mshambuliaji wake hatari Harry Kane na lapili la kusawazisha likifungwa na Eriksen dakika za lala salama.
Kikosi cha Juventus: Buffon (6), De Sciglio (7), Benatia (7), Chiellini (7), Sandro (6), Costa (7), Pjanic (8), Khedira (6), Mandzukic (7), Higuain (8), Bernadeschi (7)
Waliyokuwa benchi: Sturaro (5), Bentacur (5)
Kikosi cha Tottenham: Lloris (7), Aurier (6), Sanchez (7), Vertonghen (7), Davies (6), Dembele (8), Dier (6), Eriksen (8), Alli (7), Lamela (8), Kane (8)
Wachezaji waliyoanzia benchi: Lucas (5), Son (5), Wanyama (5)
Mchezaji bora wa mechi hiyo alikuwa ni Mousa Dembele
Share To:

msumbanews

Post A Comment: