Licha ya kupoteza mchezo wa jana kwa mabao 2-1 dhidi ya Al-Merrikh katika Ligi ya Mabingwa Afrika, Township Rollers ilifanikiwa kusonga mbele katika Ligi ya Mabingwa Afrika.

Rollers imefanikiwa kusonga mbele kutokana mechi ya awali kuibuka na ushindi wa mabao 3-0, hivyo kuwa na aggregate ya mabao 4-2.

Timu hiyo kutoka Gaborone, Botswana, sasa itakutana na Young Africans ya Tanzania katika hatua inayofuata, mchezo ukichezwa nchini, 6 March 2018, siku ya Jummane, ambapo Yanga itakuwa mwenyeji.

Yanga nayo ilifanikiwa kuwaondoa St. Louis FC ya Sychelles kwa jumla ya mabao 2-0 na kufanikiwa kupiga hatua ya kusonga mbele
Share To:

msumbanews

Post A Comment: