WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemkabidhi mbunge wa jimbo la Longido, Dkt. Stephen Kiruswa gari aina Tunland Double cabin kwa ajili ya kuboresha huduma za chanjo na afya katika jimbo hilo.

Amemkabidhi gari hilo jana (Jumatano, Februari 14, 2018) mbele ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya hiyo,  Bw. Jumaa Mhina na Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Longido, Bw. Sabore ole Moloimet.

Waziri Mkuu amesema amekabidhi gari hilo ikiwa ni utekelezaji wa ahadi aliyoitoa alipofanya ziara wilayani Longidi, Agosti, 2017. Gari la kutolea huduma za chanjo lilikuwa ni miongoni mwa changamoto zilizokuwa zinaikabili wilaya hiyo.

Kwa upande wake, Dkt. Kiruswa alitumia fursa hiyo kumshukuru Waziri Mkuu kwa niaba ya wananchi wa Halmashauri ya wilaya ya Longido. “Gari hili ni zuri sana na linahimili mazingira ya wilaya ya Longido.”

“Naishukuru sana Serikali ya Awamu ya Tano kwa kuboresha huduma mbalimbali wilayani Longido zikiwemo za afya na maji licha ya jimbo hilo kukaa muda mrefu bila ya kuwa na mbunge.”

Amesema atahakikisha gari hilo linatunzwa na linatumika kwa ajili ya matumizi yaliyokusudiwa ambayo ni huduma za chanjo na afya pamoja na huduma za mama na mtoto.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: