Articles by "BAJETIKUU2023/24"
Showing posts with label BAJETIKUU2023/24. Show all posts

 

Makamu Mwenyekiti wa kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda,Biashara,Kilimo na Mifugo Mhe.Mariamu Ditopile, akiwasilisha maoni ya kamati hiyo kwa mwaka wa fedha 2025-2026 leo Mei 14,2025 bungeni jijini Dodoma.
Makamu Mwenyekiti wa kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda,Biashara,Kilimo na Mifugo Mhe.Mariamu Ditopile, akiwasilisha maoni ya kamati hiyo kwa mwaka wa fedha 2025-2026 leo Mei 14,2025 bungeni jijini Dodoma.

Na.Alex Sonna-DODOMA

KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda,Biashara,Kilimo na Mifugo imeiomba Serikali kujitahidi kutoa elimu kuhusu lumbesa katika maeneo mbalimbali nchini,kwani bado kuna baadhi ya wafanyabiashara wasio waaminifu wameendelea kutumia mfumo huo unaowanyonya wakulima na pia unaikosesha Serikali mapato.

Ushauri huo umetolewa leo Mei 14,2025 bungeni Dodoma na Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo,Mhe.Mariamu Ditopile wakati akiwasilisha maoni ya kamati hiyo kwa mwaka wa fedha 2025-2026.

Mhe.Ditopile amesema inashauri Serikali iendelee kutoa elimu kwa wananchi sehemu mbalimbali kuhusu umuhimu wa kutumia vipimo sahihi (mizani) na athari inayopatikana kwa kutumia lumbesa.

“Serikali itoe mwongozo maalum utakaotumiwa na Halmashauri zote nchini ili kuondoa mkanganyiko 17 kuhusu matumizi ya mizani. Aidha, izitake Halmashauri zote zisimamie kwa uwiano ambao utaleta manufaa kwa wakulima,”amesema Mhe.Ditopile

Kuhusu mfumo wa Stakabadhi ghalani,Makamu Mwenyekiti huyo amesema wanaishauri Serikali Kuvisimamia Vyama vya Msingi na kuhakikisha vinawalipa Wakulima fedha zao kwa wakati mara taratibu za mauzo zinapokamilika ili kuondoa migogoro isiyo ya lazima baina ya Serikali na Wananchi.

Pia,Kuhakikisha kuwa tozo na ushuru wa mazao ya Wakulima zinapunguzwa kwa kuwa baadhi zinasababisha kero.

“Marekebisho ya tozo na ushuru yanayolenga kuwapunguzia gharama wakulima yatawapa imani zaidi wakulima hao kwa Serikali yao na hivyo kujitokeza kuuza bidhaa zao kwenye masoko halali badala ya kutumia mifumo isiyo rasmi.

Vilevile Kuendelea kutoa elimu ya uhamasishaji kwa wadau wa mfumo wa stakabadhi ghalani kuhusu kutumia mfumo rasmi kuuza na kununua bidhaa mbalimbali.
Makamu Mwenyekiti wa kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda,Biashara,Kilimo na Mifugo Mhe.Mariamu Ditopile, akiwasilisha maoni ya kamati hiyo kwa mwaka wa fedha 2025-2026 leo Mei 14,2025 bungeni jijini Dodoma.
Makamu Mwenyekiti wa kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda,Biashara,Kilimo na Mifugo Mhe.Mariamu Ditopile, akiwasilisha maoni ya kamati hiyo kwa mwaka wa fedha 2025-2026 leo Mei 14,2025 bungeni jijini Dodoma.
Na.Alex Sonna-DODOMA
KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda,Biashara,Kilimo na Mifugo imeiomba Serikali kuiongezea bajeti na kuhakikisha inatolewa yote ya Wizara ya Viwanda na Biashara ili kufanikisha Mapinduzi ya Viwanda.
Ushauri huo umetolewa leo Mei 14,2025 bungeni jijini Dodoma na Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo,Mhe.Mariamu Ditopile wakati akiwasilisha maoni ya kamati hiyo kwa mwaka wa fedha 2025-2026 ambapo amesema Kamati inaona upo umuhimu wa kuendelea kuiongezea fedha zaidi ili iweze kufikia Mapinduzi ya Viwanda yanayokusudiwa.
“Kamati inashauri Serikali kufanya yafuatayo ikiwemo iendelee kuongeza Bajeti ya Wizara hii kila mwaka ili kufanikisha Mapinduzi ya Viwanda na ihakikishe kuwa bajeti inayoidhinishwa na Bunge kila mwaka inatolewa yote kwa wakati ili shughuli zilizopangwa zitekelezeke kikamilifu,”amesema Ditopile
Pia amederma kiwango cha fedha kinachotengwa kwa ajili ya Bodi kupitia bajeti ya Serikali ni kidogo kulingana na kazi kubwa iliyopo.
Aidha, mapato ya ndani hayatoshelezi utekelezaji wa shughuli zilizopo kutokana na sehemu ndogo ya maeneo yanayotekeleza mfumo nchini na idadi ya mazao yanayouzwa kupitia mfumo wa stakabadhi za ghala.
“Kamati inaishauri Serikali kuiongezea fedha Bodi iweze kutanua wigo wa shughuli zake na kuwafikia wananchi wengi zaidi 8 kwa kuwapa elimu kuhusu matumizi ya mfumo, uhifadhi na masoko,”amesema
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe.Dkt.Selemani Jafo,akiwasilisha leo Mei 14,2025 bungeni jijini Dodoma makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2025-2026.
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe.Dkt.Selemani Jafo,akiwasilisha leo Mei 14,2025 bungeni jijini Dodoma makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2025-2026.
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe.Dkt.Selemani Jafo,akiwasilisha leo Mei 14,2025 bungeni jijini Dodoma makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2025-2026.

Na Alex Sonna-DODOMA

Wizara ya Viwand ana Biashara imepata mafanikio makubwa katika maeneo mbalimbali yakiwemo uendelezaji wa miradi ya kielezo na kimkakati; upanuzi na ujenzi wa viwanda; uendelezaji wa teknolojia mbalimbali; atamizi na ubunifu; utafutaji wa masoko ya bidhaa za Tanzania ndani na nje ya nchi; ubora wa bidhaa na ushindani wa kibiashara; na utatuzi wa migogoro.

Mafanikio hayo yametajwa leo Mei 14,2025 bungeni na Waziri wa Wizara hiyo Dkt.Selemani Jafo wakati akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2025-2026.

Waziri Jafo amesema Serikali imefanikiwa kulipa fidia ya shilingi bilioni 15.4 kwa wananchi 1,142 wanaopisha utekelezaji wa Mradi Unganishi wa Mchuchuma na Liganga.
Pia imeendelea kutekeleza miradi wa Magadi Soda Engaruka, Kufufua Kiwanda cha Kilimanjaro Mashine Tools (KMTC), Kiwanda cha Bidhaa za Kibailojia (TBPL).

Waziri Jafo amesema Katika kipindi cha miaka minne Serikali imeendelea kuweka mazingira wezeshi ili kuvutia uwekezaji wa viwanda nchini ambapo Kupitia juhudi hizo viwanda vikubwa vimejengwa na kupanuliwa vikiwemo Kiwanda cha Wild Flower and Grains Ltd; Kiwanda cha Chokaa cha Maweni (Huaxin Cement Co Ltd).

Pia Viwanda vya kuunganisha magari (Kiwanda cha GF Trucks and Equipment Ltd na Kiwanda cha Saturn Corporation Limited); Kiwanda cha kutengeneza vioo (Sapphire Float Glass (Tanzania) Company Limited); Kiwanda cha Sukari cha Kilombero; Kiwanda cha Sukari cha Mkulazi na Kiwanda cha Sukari Kagera.

Waziri Jafo amesema Serikali katika kuhakikisha inapunguza utegemezi wa uagizaji wa vifaa tiba nchini, Wizara kupitia Shirika la Uhandisi na Usanifu wa Mitambo (TEMDO) imefanikiwa kupata ithibati inayoruhusu kusanifu na kutengeneza vifaa tiba mbalimbali.
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe.Dkt.Selemani Jafo,akiwasilisha leo Mei 14,2025 bungeni jijini Dodoma makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2025-2026.
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe.Dkt.Selemani Jafo,akiwasilisha leo Mei 14,2025 bungeni jijini Dodoma makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2025-2026.
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe.Dkt.Selemani Jafo,akiwasilisha leo Mei 14,2025 bungeni jijini Dodoma makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2025-2026.

Na.Alex Sonna-DODOMA

KUPITIA Wakala wa Vipimo(WMA), Wizara ya Viwanda na Biashara imekagua na kuhakiki vipimo 1,013,859 sawa na asilimia 99.2 ya lengo la vipimo 1,022,342 vilivyopangwa kukaguliwa kwa mwaka.

Hayo yameelezwa leo Mei 14,2025 bungeni jijini Dodoma na Waziri wa Wizara ya Viwanda na Biashara,Dkt.Selemani Jafo wakati akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2025-2026.

Waziri Jafo amesema kati ya vipimo hivyo, vipimo 10,898 vilirekebishwa na vipimo 761 vilikataliwa.

Amesema WMA imeendelea kufanya kazi ya udhibiti wa bidhaa zilizofungashwa mipakani na bandarini katika vituo vya ukaguzi 13 ambavyo ni Sirari, Mtukula, Namanga, Holili, Tunduma, Tarakea, Horohoro, Kasumulu, Kwara na Bagamoyo, Manyovu, na Mbweni na Temeke.
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe.Dkt.Selemani Jafo,akiwasilisha leo Mei 14,2025 bungeni jijini Dodoma makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2025-2026.
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe.Dkt.Selemani Jafo,akiwasilisha leo Mei 14,2025 bungeni jijini Dodoma makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2025-2026.
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe.Dkt.Selemani Jafo,akiwasilisha leo Mei 14,2025 bungeni jijini Dodoma makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2025-2026.

Na.Alex Sonna-DODOMA

Wizara ya Viwanda na Biashara imeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuhakikisha bidhaa zinazozalishwa nchini zinapata masoko ya kikanda na kimataifa.

Hayo yameelezwa leo Mei 14,2025 bungeni Dodoma na Waziri wa Wizara hiyo,Dkt.Selemani Jafo wakati akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2025-2026.

Waziri Jafo amesema katika kutekeleza Mfumo Rahisi wa Ufanyaji Biashara kwa Wafanyabiashara Wadogo (STR) wanaovuka mipaka ya Tanzania na Zambia, jumla ya bidhaa 51 zilikubalika kuingia katika mfumo rahisi wa ufanyaji biashara kwa wafanyabiashara wadogo wanaovuka mpaka wa Tanzania na Zambia kutoka bidhaa 22 za awali.

Amesema bidhaa hizo mpya ni pamoja na maharage, njegere, matunda mbalimbali, viazi mviringo, soya na mboga mboga za kukausha. Aidha, kwa upande wa Tanzania na Malawi, majadilino ya uwili ya kuanzisha Mkataba wa Taratibu Zilizorahisishwa za Kiforodha.

“ Jumla ya bidhaa 61 za viwandani na kilimo zilikubalika kuingia katika mfumo huo wa STR; Ukomo wa thamani ya bidhaa wa dola za Marekani 2000 umekubalika; na Idadi ya uvukaji usio na ukomo usiozidi ukomo wa thamani hiyo umekubalika pia,”amesema Waziri Jafo
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe.Dkt.Selemani Jafo,akiwasilisha leo Mei 14,2025 bungeni jijini Dodoma makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2025-2026.
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe.Dkt.Selemani Jafo,akiwasilisha leo Mei 14,2025 bungeni jijini Dodoma makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2025-2026.
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe.Dkt.Selemani Jafo,akiwasilisha leo Mei 14,2025 bungeni jijini Dodoma makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2025-2026.

Na.Alex Sonna-DODOMA

WIZARA ya Viwanda na Biashara imepanga kutekeleza vipaumbele saba katika bajeti ya 2025-2026 ikiwememo kuwezesha uanzishwaji na uendelezaji wa Viwanda nchini.
Vipaumbele hivyo vimetajwa leo bungeni Mei 14,2025 na Waziri wa Wizara hiyo,Selemani Jafo wakati akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2025-2026.

Waziri Jafo amevitaja vipaumbele vingine ni kuendelea na utekelezaji wa miradi ya kielelezo na kimkakati,kuimarisha uwezo wa uzalishaji viwandani na utoaji huduma kwa kuboresha mazingira wezeshi ikiwa ni pamoja na ujenzi wa miundombinu ya mitaa ya viwanda (Industrial Clusters) kwa ajili ya viwanda vidogo na vya kati.

Pia, Kuboresha mazingira ya biashara na kuchochea ukuaji wa Sekta binafsi;Kuendelea na utafutaji wa masoko kwa bidhaa na huduma zinazozalishwa nchini; Kuchochea Maendeleo ya watu kwa kuboresha miradi na programu kwa Jamii inayohusisha elimu na Mafunzo ya Ujuzi.
Kipaumbele kingine ni Kuimarisha Usimamizi wa Ubora na Usalama wa Bidhaa Nchini zikiwemo bidhaa za chakula na vipodozi.

 Kwa kauli moja leo tarehe 13 Mei 2025 Bunge la Tanzania limepitisha kwa kishindo bajeti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na Taasisi zake kwa mwaka 2025/2026 yenye jumla ya shilingi Trilioni 2.439.


Bajeti hiyo imepitishwa kwa asilimia 100 na wabunge ili kuwezesha utekelezaji wa malengo yaliyoanishwa kwa mwaka wa fedha 2025/26, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na Taasisi zake.

Kati ya fedha hizo zilizopitishwa jumla ya shilingi Bilioni 688.6 ni kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida ya Wizara ambapo Shilingi Bilioni 635.2 ni kwa ajili ya Mishahara na Shilingi Bilioni 53.3 ni kwa ajili ya Matumizi Mengineyo.

Utekelezaji wa bajeti hiyo utajikita zaidi katika maeneo matano ya vipaumbele ambayo ni i) kuendelea na utekelezaji wa Sera na Mitaala, Mapitio ya sheria, Uandaaji wa miongozo, na utoaji wa mafunzo, ii) Kuongeza fursa na kuimarisha ubora wa mafunzo ya Amali katika shule za sekondari na vyuo vya Amali, iii) Kuongeza fursa na kuimarisha ubora wa elimu ya Amali, Msingi, Sekondari na Ualimu, iv) Kuongeza na kuimarisha ubora wa elimu ya juu na v) Kuimarisha uwezo wa nchi katika utafiti, Matumizi ya Sanyansi, Teknolojia na Ubunifu ili kuchangia upatikanaji wa maendeleo endelevu.

Wabunge wamempongeza Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof Adolf Mkenda (Mb) kwa utulivu wa kiutendaji katika wizara yake na mshikamano alionao na watendaji wote wa Wizara na kumsihi kusimamia kwa weledi mkubwa wizara hiyo ambayo ni msingi wa maendeleo ya nchi.

Kati ya fedha zilizopitishwa, zaidi ya shilingi Trilioni 1.7 ni kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo ambapo Shilingi 1.186 ni fedha za ndani na Shilingi 560.8 ni fedha kutoka kwa Washirika wa Maendeleo.

Kwa mujibu wa Waziri Mkenda, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kupitia Tume ya Taifa ya UNESCO imeidhinishiwa jumla ya Shilingi Bilioni 3.2 kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida ambapo Mishahara ni Shilingi Bilioni 1.5 na Matumizi Mengineyo ni Shilingi Bilioni 1.7

Waziri Mkenda amesema kuwa jumla ya wabunge 36 wamechangia moja kwa moja huku wengine wakichangia kwa maandishi ambapo wote kwa pamoja wameshauri na kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kwa mageuzi makubwa ya pili ya elimu sambamba na ongezeko kubwa la bajeti.

Pia Waziri Mkenda amesema kuwa wabunge wote waliochangia pia wamempongeza Rais Samia kwa kuongeza mikopo elimu ya juu, ongezeko la Vyuo vya Ufundi stadi-VETA, Ujenzi na ongezeko la shule za Amali pamoja na Ujenzi wa kampasi mpya za vyuo vikuu.






 


Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde ameainisha vipaumbele vya Wizara ya Madini kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026, ambako imelenga kuimarisha mchango wa Sekta ya Madini katika kukuza uchumi wa taifa, kuongeza ajira, na kuinua ustawi wa jamii kupitia matumizi bora ya rasilimali za madini hapa nchini.

Ameyabainisha hayo leo Mei 02, 2025 Bungeni Jijini Dodoma wakati akiwasilisha Hotuba ya Mpango wa Mapato na Matumizi ya Wizara ya Madini kwa Mwaka wa Fedha wa Serikali wa 2025/2026 ambapo kupitia mpango huo, Wizara ya Madini imepanga kukusanya maduhuli ya shilingi 1,405,537,268,755.00 (Trilioni 1.4).

Ili kufikia lengo hilo la makusanyo ya maduhuli, Waziri Mavunde amebainisha kuwa, Wizara imeweka mkazo kwenye kuimarisha ukusanyaji wa maduhuli ya Serikali kwa kuhakikisha mifumo ya ukusanyaji mapato inaendelea kuwa ya kisasa, shirikishi sambamba na yenye uwazi. 

Waziri Mavunde amesema kuwa, hatua hiyo, inakwenda sambamba na lengo kuu la kuongeza mchango wa Sekta ya Madini kwenye Pato la Taifa (GDP) hususan kupitia ongezeko la shughuli za uongezaji thamani na mauzo ya madini ndani na nje ya nchi. Itakumbukwa kuwa mchango wa Sekta kwenye GDP umefikia asilimia 10.1 mwaka 2024 ikiwa ni mwaka mmoja kabla ya muda ulioainishwa katika Sera ya Madini ya Mwaka 2009 na kwenye Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa miaka mitano 2021/2022 hadi 2025/2026. 

Aidha, Waziri Mavunde ameeleza kuwa, Vipaumbele hivyo pia vinaangazia kuendeleza mnyororo wa thamani kwenye madini muhimu na mkakati kama vile madini ya kielektroniki, ambayo yanatajwa kuwa nguzo ya maendeleo ya teknolojia duniani ambako kwa kufanya hivyo, Tanzania inalenga kujenga uchumi shindani unaotegemea maarifa na ubunifu.

Ameongeza kuwa, Wizara imedhamiria kuhamasisha uwekezaji katika Sekta ya Madini, huku kipaumbele kikiwa ni uongezaji thamani ndani ya nchi kabla ya kusafirishwa na kuuzwa nje ya nchi. Aidha, kuimarisha uendeshaji wa minada na maonesho ya madini ya vito ni hatua inayolenga kuongeza uwazi, ushindani, na thamani halisi ya madini yanayouzwa.

Sambamba na hilo, katika jitihada za kuhakikisha rasilimali za madini zinatumika kwa tija, Waziri Mavunde amesisitiza kuwa Serikali imepanga kuongeza uwekezaji kwenye tafiti za kina za madini, kwa kushirikiana na taasisi za kitaaluma na sekta binafsi, hatua itakayowezesha kugundua maeneo mapya ya uchimbaji, kuandaa ramani sahihi za kijiolojia pamoja na kuimarisha kanzidata ya jioliojia ya nchi.

Kwa kutambua mchango wa wachimbaji wadogo, Waziri Mavunde ameeleza kuwa, mpango huo umeweka kipaumbele cha kuwarasimisha na kuwaendeleza wachimbaji hao, kwa kuwapatia elimu, teknolojia, kuwaunganisha na taasisi za kifedha ili kupata mikopo yenye masharti nafuu kukuza mitaji yao na kuendelea kuwa masoko ya uhakika ili waweze kufanya kazi zao kwa ufanisi, usalama na tija.

Pia, Waziri Mavunde amesisitiza kuwa, Serikali kupitia Wizara itaendelea kuzijengea uwezo taasisi zilizo chini ya Wizara ya Madini kama Tume ya Madini, Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini (GST) Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), Kituo cha Jemolojia Tanzania (TGC) pamoja na Taasisi ya Uhamasishaji na Uwazi katika rasilimali Madini, Mafuta na Gesi Asilia (TEITI) ili kusaidia kuboresha usimamizi, utafiti na uwekezaji katika sekta hiyo muhimu kwa maendeleo ya taifa.

Bajeti ya Wizara ya Madini kwa Mwaka 2025/2026 inalenga kujenga Sekta ya Madini imara, endelevu na shindani kimataifa kwa kuwa ni moja kati ya sekta inayozalisha ajira, kuongeza mapato ya serikali, na kuchochea maendeleo na miundombinu nchini, maendeleo ya kijamii na uchumi kwa ujumla.







Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan ameitaka Wizara ya Nishati na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO)  kuhakikisha mradi wa njia kuu  ya kusafirisha umeme kutoka Tabora hadi Katavi (132kV)  pamoja na ujenzi wa kituo cha kupokea, kupoza na kusambaza umeme vinakamilika kwa wakati ili  Mkoa wa Katavi uingizwe kwenye gridi ya Taifa ifikapo mwezi Septemba mwaka huu.

Mhe. Dkt.Samia ameyasema hayo leo 13 Julai, 2024 wakati alipokuwa akizungumza  na wananchi wa Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi mara baada ya kukagua maendeleo ya mradi wa njia kuu ya kusafirisha umeme wa msongo wa kilovoti 132 wa Tabora-Katavi  na kituo cha kupokea, kupoza na kusambaza umeme cha Inyonga ambapo ameridhika na maendeleo ya miradi hiyo.

‘’Natamani Katavi iachane kabisa  na matumizi ya Majenereta ambayo ni gharama kubwa na pia kukamilika kwa miradi hii kutawawezesha wananchi wa Katavi kuutumia umeme kwa maslahi ya kiuchumi na kukuza uwekezaji,  Serikali imetumia gharama kubwa kutekeleza miradi hii  nawaasa wananchi mchangamkie fursa zinazotokana na kuwepo kwa umeme wa kutosha na wa uhakika." Amesema Dkt.Samia

Aidha,  amepongeza kazi nzuri inayofanywa na TANESCO katika  kutekeleza miradi ya umeme na kuwataka kuongeza kasi kwenye uunganishaji wa wateja pindi miradi inapokamilika.

Amesisitiza kuwa,  umeme ni tegemeo kubwa kwa watu binafsi pamoja na uchumi wa viwanda na hiyo yote ni utekelezaji wa  Ilani ya Chama cha Mapinduzi ambayo inaelekeza  uwepo wa umeme wa kutosha nchini.

Aliwasilisha taarifa ya utekelezaji kwa  Mhe.  Rais, Mkurugenzi Mtandaji wa  Shirika la  Umeme Tanzania TANESCO Mha. Gissima Nyamo-Hanga amesema, mradi huo pindi utakapokamilika utaokoa kiasi cha takribani Bilioni 2.2  kwa mwezi kwa ajili ya mafuta yanayotumika kuendesha Mitambo ya Umeme inayotumiwa mkoani Katavi pindi tu itakapoingizwa kwenye umeme wa Gridi ya Taifa

 Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amemuagiza Mkandarasi Avic anayejenga barabara ya mzunguko wa nje ya Dodoma, yenye urefu wa Kilometa 112.3 sehemu ya Ihumwa Dry Port - Matumbulu - Nala (km 60), kuhakikisha anakamilisha barabara hiyo ifikapo mwezi Desemba, 2024.

Bashungwa ametoa agizo hilo Septemba 29, 2023, jijini Dodoma wakati akikagua maendeleo ya ujenzi wa barabara hiyo ambapo pamoja na mambo mengine amemsisitiza mkandarasi huyo kuongeza spidi kwenye ujenzi wa madaraja mawili ambayo yanaonekana kuchelewa ujenzi wake.

“Sipepesi macho kwenye usimamizi wa mikataba, kufanya kazi kwa ubora na kasi ndio kipimo chako, ukizembea kwenye kazi hii usahau kupewa kazi nyingine za ujenzi kwenye Sekta hii nchini”, amesema Bashungwa.

Ameahidi kutembelea tena mradi huo ifikapo Desemba mwaka huu ili kuona uetekelezaji wa maagizo yake na kumsisitiza Mkandarasi huyo kufanya kazi usiku na mchana ili uweze kukamilika kwa wakati kulingana na maelekezo ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Aidha, Bashungwa ameuagiza Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS), kushirikiana na Shirika la Reli (TRC), kurudisha haraka mawasiliano ya barabara ya lami eneo la Mkonze na Nala ambalo lilibomolewa kwa ajili ya ujenzi wa reli ya SGR kwani wananchi wamekuwa wakipata kero kutokana na changamoto katika maeneo hayo.

Bashungwa amewataka wakandarasi nchini wanaotekeleza miradi ya ujenzi kuhakikisha wanatekeleza miradi hiyo kwa mujibu wa Mkataba na kusisitiza kutokuwa na huruma kwa yeyote atakayekiuka mikataba hiyo.

Bashungwa amemuagiza Mhandisi Mshauri Mzawa wa kampuni ya Inter-Consult kumsimamia mkandarasi wa kampuni ya China Civil Engineering Corporation (CCEC) anayetekeleza sehemu ya Nala - Veyula - Mtumba (km 52.3), kutoa vifaa vya usalama kwa wafanyakazi wake ili kuepukana na madhara yanayoweza kutokea maeneo ya kazi.

Katika hatua nyingine, Bashungwa amewaagiza Mameneja wa TANROADS wa mikoa yote nchini kuhakikisha wanazibua mifereji ya barabara zilizo chini ya Wakala huo kabla ya mvua hazijaanza ili zisiwe chanzo cha kuleta mafuriko, sambamba na hilo Waziri huyo amempongeza Meneja wa TANRODS Mkoa wa Dar es Salaam kwa kufanya matengenezo na kuzibua barabara na mifereji katika mkoa huo.

Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa TANROADS, Eng. Mohamed Besta ameeleza kuwa mpaka sasa sehemu ya mradi kutoka Nala – Veyula – Mtumba (km 52.3) umefika asilimia 54.3 na sehemu inayoanzia Ihumwa Dry Port – Matumbulu – Nala umefika asilimia 50 na sasa wakandarasi wanaendelea na kazi mbalimbali za ujenzi wa makalavati na madaraja makubwa mawili.

Mradi wa Barabara ya Mzunguko wa nje ya Dodoma (Km 112.3), unagharimiwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) kwa gharama ya shilingi Bilioni 221 na unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba 2024.


Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa, akitoa maelekezo kwa mkandarasi wa Kampuni ya Avic wakati alipokagua maendeleo ya ujenzi wa barabara ya mzunguko wa nje ya Dodoma yenye jumla ya urefu wa kilometa 112.3; sehemu ya Ihumwa Dry Port - Matumbulu - Nala (km 60), Septemba 29, 2023 jijini Dodoma.

 Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa, akiangalia kiatu cha mmoja wa Wafanyakazi katika mradi wa ujenzi wa barabara ya mzunguko wa nje ya Dodoma yenye urefu wa kilometa 112.3; sehemu ya Nala -Veyula – Mtumba (km 52.3), Septemba 29, 2023 jijini Dodoma. Amemsisitiza Mkandarasi China Civil Engineering Corporation kuwanunulia vifaa vya usalama wafanyakazi wake.

Muonekano wa sehemu ya barabara ya mzunguko wa nje ya Dodoma (km 112.3) inayojengwa kwa kiwango cha lami. Ujenzi wake unagharimiwa na Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) kwa gharama ya shilingi Bilioni 221.