Na Mwandishi Wetu
MAKAMU wa Rais wa Tanzania, Deogratius Ndejembi, ametoa maeekezo kwa Wizara ya Viwanda na Biashara kukaa meza moja na wazalishaji wa saruji nchini ili kuweka mikakati ya haraka itakayohakikisha saruji inapatikana kwa wingi na bei nafuu.
Ametoa maelekezo jijini Dar es Salaam alipokuwa katika hafla ya utoaji wa Tuzo za Rais kwa Mzalishaji Bora Viwandani (President’s Manufacturer of the Year Awards - PMAYA), zinazoratibiwa na Shirikisho la Wenye Viwanda Tanzania (CTI).
Akieleza kero ya wananchi kuhusu gharama za ujenzi, Makamu wa Rais amesema kwamba wananchi wanalazimika kununua saruji kwa bei kubwa kutokana na usimamizi na uratibu dhaifu wa uzalishaji viwandani, jambo ambalo linaenda kinyume na maelekezo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Kutokana na bei ya saruji kuwa juu Makamu wa Rais Ndejembi amesema” Nakuagiza Waziri wa Viwanda na Biashara, Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda pamoja na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kaeni mmalize hili suala ili mwananchi apate saruji kwa bei iliyokuwepo awali.



Post A Comment: