Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mheshimiwa Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.), amekutana na kuagana na Balozi wa Umoja wa Ulaya nchini Christine Grau, kufuatia kukamilika kwa muda wake wa uwakilishi nchini.

Katika mazungumzo yao, Mheshimiwa Waziri Kombo alimpongeza Balozi Grau kwa mchango wake katika kuendeleza mahusiano kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya, hususan katika maeneo ya ushirikiano wa maendeleo, biashara na uwekezaji, Global Gateway, sekta binafsi, pamoja na majadiliano ya wazi kati ya pande hizo mbili.

Ameelezea azma ya Tanzania kuendelea kushirikiana na Umoja wa Ulaya katika misingi ya kuheshimiana, uwazi na manufaa ya pande zote, huku akimtakia Balozi Grau kila la kheri katika majukumu yake yajayo.

Kwa upande wake, Balozi Grau aliishukuru Serikali ya Tanzania kwa ushirikiano alioupata katika kipindi cha uwakilishi wake nchini, na kusisitiza umuhimu wa kuendeleza ushirikiano wa kimkakati kupitia majadiliano ya wazi na ushirikiano wa katika sekta muhimu maendeleo, kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya.
Share To:

OSCAR ASSENGA

Post A Comment: