Nilimpenda sana. Zaidi ya kupenda, nilimheshimu na kumchukulia kama rafiki wa kweli. Tulikuwa tumekutana kazini, na kuanzia siku ya kwanza alipoomba namba yangu, nilihisi kuna kitu cha kipekee. Mahusiano yetu yalianza kwa kasi nzuri, tukawa tukizungumza kila saa, tukitoka pamoja, na hata kupanga mambo ya baadaye kwa ujasiri.
Lakini miezi michache baadaye, kila kitu kilianza kubadilika. Simu zangu zilianza kujibiwa kwa mkato. Ujumbe nilimtumia saa tatu asubuhi ulijibiwa saa mbili usiku, na mara nyingi bila hata salamu. Nilipojaribu kuanzisha mazungumzo ya undani, alikua mwepesi wa kusema, “niko busy,” “leo nimechoka,” au “tutazungumza baadaye.”
Nilianza kubaki peke yangu kwenye mipango yetu ya kawaida. Outing zilizokuwa kawaida ya kila wiki zikageuka kumbukumbu. Badala ya lunch pamoja, nilikula peke yangu ofisini. Badala ya jumamosi ya kutembea, alikua na ‘harusi ya binamu’ au ‘kazi ya dharura.’ Sikujua kama alikuwa ananicheza au kuniacha polepole.
Ilikuwa inaniuma sana. Wakati mwingine nilijikuta nikilia usiku, nikiwaza nilikosea wapi. Nilijitahidi kuwa mpenzi bora, nilitoa muda, nilielewa majukumu yake ya kazi, lakini bado nilihisi kana kwamba sipendwi tena. Kibaya zaidi, alikataa hata kusema kama hataki tuendelee alikua akiniacha nikiwa kwenye ukimya wa mateso. Soma zaidi hapa
Post A Comment: