Wakati mwingine maneno ya watu yanaweza kukukata tamaa kabisa, hasa pale yanapotoka kwa wale unaowaamini. Kuna wakati nilikuwa naishi kama kivuli cha kile nilichotamani kuwa.
Nilikuwa nikijitahidi kuvaa vizuri, kuongea kwa heshima, hata kushiriki matukio ya kijamii kwa adabu zote lakini bado, nilihukumiwa kwa sura, mavazi, na hali yangu ya maisha.
Mara kwa mara, ningeambiwa kwamba mimi ni wa “level ya chini”, kwamba sina mvuto, kwamba hata nikijitahidi nitabaki kuwa wa kawaida. Wengine walidiriki kunisema hadharani: “Yule mama anaonekana cheap, hana class kabisa.”
Hapo ndipo nilianza kuamini labda kuna kitu ndani yangu ambacho hakivutii, au labda nilizaliwa bila mvuto wa kipekee kama wanawake wengine. Maisha yangu ya ndoa nayo hayakuwa na ladha.
Mume wangu alikuwa mzito kuniangalia, hata akinisifia ilikuwa kama kwa huruma tu. Nilikuwa na watoto wawili, na hata kwenye familia yangu, walinikumbuka kwa kazi, si kwa uzuri au haiba. Nilianza kujiuliza: hivi mimi nina mapungufu ya asili? Soma zaidi hapa
Post A Comment: