Neema Lugangira aliyekuwa Mbunge Viti Maalum CCM - Kundi la NGOs amechukua Fomu ya Kugombea Ubunge wa Viti Maalum NGOs katika Uchaguzi ujao 2025. 

Lugangira anatetea nafasi aliyoitumikia katika Bunge la 12, 2020-25 kwa mafanikio makubwa yaliyopelekea CCM kuongeza nafasi ya Uwakilishi kwa Kundi hili kutoka kuwa moja Tanzania Bara na moja Zanzibar hadi sasa ni nafasi mbili kwa upande wa Tanzania Bara na nafasi moja kwa upande wa Zanzibar.

Fomu hizo amekabidhiwa leo tarehe 28 Juni na Mkuu wa Idara ya UWT Taifa ya Oganaizesheni, Itikadi na Uhusiano wa Kimataifa, Ndg. Mary Mwenisongole katika Ofisi za Makao Makuu ya UWT, Dodoma.




Share To:

Post A Comment: