Na Denis Chambi, Tanga.

TAASISI ya Kuzuia na kupambana na Rushwa 'TAKUKURU' Mkoa wa Tanga imefanikiwa kuokoa fedha kiasi cha zaidi ya shilingi Milioni 76 ambazo ni makusanyo ya mapato ya halmashauri za wilaya za Tanga , Kilindi na Korogwe ambapo watumishi walilopewa dhamana ya kuzikusanya walikosa uadilifu.

Akitoa taarifa ya kipindi cha mwezi Oktoba hadi December  2024 mbele vya vyombo vya habari Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Tanga  Ramadhani Ndwatah amesema kuwa baada ya kufanya uchunguzi walibaini uwepo wa baadhi ya watumishi waliokuwa wakikusanya fedha hizo kinyume na mfumo na hatimaye kuwafikisha Mahakamani ambapo waliamriwa kuzirejesha.

"Miongoni mwa kazi tulizozifanya  kwa kipindi hiki tulibaini taarifa za tuhuma za ubadhilifu na ufujaji wa  fedha na mali za umma , tuliwafikisha mahakamani watuhumiwa kwa tuhuma za ubadhilifu wakiwa ni watumishi  wa umma na Jamhuri ilishinda kesi ambapo waliamriwa na Mahakama kurejesha fedha kiasi cha shilingi  Milion 76,048,459.21"

"Katika wilaya ya Kilindi kufuatia Jamhuri kushinda kesi fedha ambazo ni mapato ya Serikali kiasi cha 58,678,780.00 zilirejeshwa, wilayani Korogwe fedha kiasi cha 9,198,045.31 zilirejeshwa ambapo mbali na kurejesha fedha hizo watuhumiwa walipatiwa adhabu nyingine" alisema Ndwatah  na kuongeza..

"Katika Jiji la Tanga Jamhuri ilishinda kesi za uhujumu uchumi  jumla ya shilingi Bilion 3,171,633.9 zilizofanywa ubadhilifu kwenye utekelezaji wa miradi ya maendeleo  katika sekta ya elimu  na shilingi 5,000,000 ya mikopo ya asilimia 10 ya wanawake vijana wa watu wenye ulemavu fedha hizo zilirejeshwa na watuhumiwa kwa amri ya Mahakama sambamba na adhabu nyingine."

Aidha  Ndwatah ameeleza kuwa TAKUKURU katika kutekeleza jukumu lake la kiuchunguzi  imepokea jumla ya taarifa 120 ambapo kati ya hizo 82 zilihusu vitendo vya rushwa  na 38 hazikuhusiana na vitendo vya rushwa  huku 76 zikiendelea  kuchunguza wakati huo huo 38 zimefungwa na nyingine 6 zikihamishiwa  idara nyingine.

Ndwatah ameongeza kuwa TAKUKURU Mkoa wa Tanga imejipanga katika kipindi cha January hadi Marchi 2025 kuendelea kufwatilia miradi ya maendeleo ikiwemo ya Barabara ,huku ikichukua hatua kali za kisheria ili kudhibiti mianya ya rushwa.

" Mikakati yetu ni kuendelea kufwatilia utekelezaji wa  miradi ya maendeleo  ikiwemo miundombinu ya Barabara na mingineyo , tutaendelea kufanya udhibiti na uzuiaji kwenye eneo la ukusanyaji wa mapato  kwa kushirikiana na mamlaka husika.

Mkuu huyo wa  TAKUKURU Mkoa wa Tanga amewataka wananchi na jamii kwa ujumla kuendelea kuwa wazalendo kwa   kutoa ushirikiano pale wanapoona viashiria vya rushwa  kutoa taarifa kwenye Mamlaka husika.

"Ninatoka wito kwa wadau wote  kuendelea kutekeleza kauli mbiu yetu isemayo  kuzuia rushwa ni jukumu lako na langu  hivyo ni jukumu la kila mmoja wetu kuhakikisha anazuia vitendo vya rushwa katika eneo lake" alisema.

Katika hatua nyingine taasisi ya kuzia na kupambana na rushwa "TAKUKURU " Mkoa wa Tanga imefanikiwa kuwafikia wananchi 1,489,269  kupitia mikutano ya hadhara , maeonyesho mbalimbali , mashuleni , watoa huduma wakiwemo watumishi wa Serikali ikiwa ni mkakati wake kwa jamii kueleza kuhusu athari za kutoa na kupokea rushwa .

Share To:

Post A Comment: