Katibu wa NEC - Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM Taifa Ndugu. Amos Makalla ambaye pia ni Mlezi wa Mkoa wa Dar es salaam (kichama) akizungumza katika Ukumbi wa Diamond Jubilee ambapo Leo amepokelewa na Umati wa WanaCCM .

Mwenezi Makalla amesema Kumezuka suala la Watu kupigiana chapuo yaani "... unakuta Wilaya nzima wanakuwa na ajenda na Mtu, wanaimba Mitano tena kwa Diwani ama Mbunge kumbe ni ajenda, na wanaacha kabisa Chama, unakuta anapigiwa chapuo mtu mmoja, sasa nami nielekeze suala  hili la Mitano tena liwe kwa Mwenyekiti wetu, wengine tufuate Utaratibu kwani ndivyo tulivyowekeana Taratibu."






Share To:

Post A Comment: