Na Joel Maduka ,Geita

Mjumbe wa Halmashuri kuu ya CCM Taifa ,  MNEC Chacha Wambula (WAJA) akiwa wilayani Bukombe Mkoani Geita amewataka vijana kutojiingiza katika Makundi yasiyofaa kwani yanaweza kuleta athari Kubwa  kwenye Jamii.

 Hayo ameyasema wakati alipokuwa akifunga Makambi ya Umoja wa Vijana  wa CCM (UVCCM)  wilaya ya Bukombe yaliyodumu kwa kipindi cha siku sita Wilayani humo huku akiwataka vijana hao kuzingatia  yale yote waliyofundishwa yaweze kuwa na  tija kwa Jamii na pamoja na chama cha Mapinduzi(CCM).

 Aidha Mnec Chacha amewataka vijana kuzingatia suala zima la uzalendo kwa Nchi na kutangaza matendo mema ambayo yamefanywa na Serikali ya awamu ya sita(6),huku akisisitiza uwajibikaji na uchapakazi kwa vijana.

 “Niwaombe vijana wangu najua hapa mmefundishwa mambo mbalimbali yakiwemo ya ujasiriamali nendeni mkatumie yale ambayo mmefundishwa kwenda kuanzisha miradi ya kiuchumi mimi nipo tayari kuwasapoti wale ambao wataitaji msaada wangu”Amesema Chacha Wambura.

 “Mimi nimaamini katika vitu vitatu uchapakazi,kuwa mwaminifu na kuwa muwazi kama unavitu hivi leo hii uwezi kukosa kazi lakini kama wewe kitu kimoja wapo kinakosekana hata ukifanya kazi utaondolewa kazini,Elimu ni kitu kingine unaweza kuwa na elimu na ukakosa hivi vitu elimu yako isikusaidie”amesema Chacha Wambura.

 Aidha Mnec Chacha amewaomba vijana kujifunza desturi ya utii  kwani sio utumwa kwa kijana kuwa mtii na kuheshimu mamlaka muhimu ambazo zimewekwa na Nchi pamoja na serikali.



Share To:

JOEL MADUKA

Post A Comment: