Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Aretas Lyimo ameshiriki katika sherehe za uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru zilizofanyika katika Uwanja wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU) mkoani Kilimanjaro.

Mgeni rasmi katika uzinduzi wa Mbio za Mwenge mwaka 2024 alikuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa ambaye amewaasa watumiaji wa bangi kuacha mara moja kwa ustawi wa maisha yao na taifa kwa ujumla.

Pia, amewaonya wakulima wa bangi nchini kuachana na Kilimo hicho na watakao kaidi hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao. Sambamba na hilo, Mhe.Majaliwa amewaomba viongozi wa dini, Taasisi za Umma na binafsi, wazazi na walezi kushiriki  katika malezi ya vijana na kutoa elimu juu ya madhara ya biashara na matumizi ya dawa za kulevya kwa jamii.

Share To:

Post A Comment: