Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Dkt. Emmanuel John Nchimbi, akiendesha Kikao cha Sekreterieti ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC), iliyofanyika leo Jumanne, Januari 16, 2024, Ofisi Kuu ya CCM Zanzibar, iliyoko Kisiwandui, Unguja, ikiwa ni siku moja baada ya kuteuliwa na NEC ya CCM Taifa kushika nafasi hiyo ya Mtendaji Mkuu wa Chama, ambapo baada ya kukaribishwa ofisini na kutia saini, alipata wasaa pia wa kufanya mazungumzo na Manaibu Katibu Mkuu wa CCM, Ndugu Anamringi Macha (Bara) na Ndugu Mohammed Said Mohammed Dimwa (Zanzibar).




 

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Dkt. Emmanuel John Nchimbi, akiwasili Ofisi Kuu ya CCM Zanzibar, iliyopo Kisiwandui, Unguja, leo Jumanne, Januari 16, 2024, tayari kuendelea na kazi, siku moja baada ya kuteuliwa na Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC) kushika nafasi hiyo ya Mtendaji Mkuu wa Chama, ambapo baada ya kukaribishwa na Manaibu Katibu Mkuu, Ndugu Anamringi Macha (Bara) na Ndugu Mohammed Said Mohammed Dimwa (Zanzibar) na kutia saini, ameendesha Kikao cha Sekreterieti ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, iliyofanyika ofisini hapo.

Share To:

Post A Comment: