Wanafunzi zaidi ya 1,000 wa shule za msingi, sekondari na vyuo wilayani Babati mkoani Manyara wamepewa mafunzo maalum ya kudhibiti dawa za kulevya kutoka Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa hizo nchini (DCEA) Kanda ya Kaskazini.

Mamlaka hiyo imeamua kuwekeza katika kutoa elimu ya dawa za kulevya kwa wanafunzi ili kuwawezesha kutimiza ndoto walizonazo kwani kundi kubwa linalotumbukia kwenye matumizi ya dawa hizo ni vijana ambao wengi wao wapo mashuleni na vyuoni.

Afisa ustawi wa jamii kutoka mamlaka ya kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya Kanda ya kaskazini Sarah Ndaba, amesema mafunzo hayo yametolewa na mamlaka hiyo kwa kushirikiana na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) mkoa wa Manyara, wakiamini kuwa itakuwa chachu kwa wanafunzi, walimu na wananchi kwa ujumla kushiriki katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya na rushwa.

Share To:

Post A Comment: