Sehemu ya Watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga-Bombo wakiwa za zawadi zao za sikuuu ya Christmas ambazo zimetolewa na Uongozi wa Hospitali hiyo
Na Oscar Assenga,Tanga
UONGOZI wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga-Bombo umetoa zawadi za sikuu ya Krismas kwa wafanyakazi wake ikiwa ni utamaduni wao wa kila sikuu kubwa kufanya hivyo.
Zoezi la Ugawaji huo lilifanywa na Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Dkt Naima Yusuf ambaye alisema ni muhimu wafanyakazi kusherehekea sikuuu kwa amani na utulivu.
Alisema ugawaji wa zawadi hizo ni zoezi ambalo limekuwa likifanyika katika sikuu za Eid na Krismas lengo likiwa ni kutoa motisha kwa watumishi katika Hospitali hiyo.
Aidha aliwataka kuendelea kuchapa kazi kwa waledi na uaminifu mkubwa katika kuwahudumia wagonjwa wanaofika kupataa huduma mbalimbali.
Akizungumza kwa niaba ya Watumishi wa Kitengo cha Maabara katika Hospitali hiyo Salvatory Lyimo alisema wana mshukuru Mganga Mfawidhi Dkt Naima Yusuf kwa zawadi hiyo aliyowapa wafanyakazi sikuu zitaenda kuwa nzuri endelee kuwa na moyo huo huo kuwajali.
Alisema aliushukuru uongozi kwa zawadi hizo ambazo wamekuwa wakizitoa kila sikuuu wanawalisha Mungu awabariki na kuwapa maisha mazuri.
Post A Comment: