Afisa Utamaduni Mkoa wa Mbeya Victoria Shao akizungumza katika kikao maalumu kilichowahusisha Wasanii, Waigizaji na waimbaji kilicho andaliwa na Wizara ya Utamadunim Sanaa na Michezo.

............................................................

Na Mwandishi Wetu Mbeya

 

KIASI cha Shilingi Bilioni 5 kimetengwa na mfuko wa wizara ya sanaa na utamaduni ili kuwawezesha wasanii na waigizaji wa "Bongo Movie" wa mkoa wa Mbeya.

Akizungumza katika kikao maalumu kilichowahusisha Wasanii, Waigizaji na waimbaji wa mkoa wa Mbeya na Songwe Afisa Mtendaji Mkuu [CEO] wa mfuko huo Nyakaho Mahemba amesema Wizara imeanza kutoa fedha hizo kwa wasanii kuanzia Desemba 2022 ambapo  imelenga kukuza na kuendeleza kazi za wasanii kujiendesha kibiashara badala ya burudani pekee.

Mahemba amesema katika mpango wa serikali ni kuongeza ajira na kuongeza mitaji kwa wasanii kupitia mafunzo na kuongeza ubora  wenye lengo la kukidhi soko la ndani na nje ya nchi.

Amefafanua kuwa wasanii wana uwezo wa kukopa mtaji kuanzia Shilingi laki 2 hadi Shilingi Mil 100 ili kufikia malengo na kwamba mfuko wa Utamaduni unashirikiana na mabenki ili kuwezesha mikopo ya Wasanii.

Afisa mtendaji Mkuu huyo ameendelea kusema kuwa tayari imeshatolewa mikopo kwa awamu mbili, mwezi Desemba 2022 na mkopo wa pili umetolewa Mwezi Februari ambapo tayari  jumla ya Shilingi Bil 1.077 kwa miradi 45 na hivyo kuzalisha ajira 88,750.

Kwa upande wake Afisa Utamaduni wa mkoa wa Victoria Shao amesema mikopo hiyo ya wasanii itachangia ajira na kuwasaidia kuwainua kiuchumi ambapo wasanii,waimbaji,wabunifu wa kazi za mikono,Waandishi wa kazi za kifasihi na wachoraji wanapaswa kuchangamkia fursa hiyo.

Shao amesema serikali itakuwa karibu na wasanii kwa maelekezo na elimu ya mikopo ili waweze kukopa kurejesha ili iweze kuwanufaisha wasanii wengine.

 Afisa Mtendaji Mkuu [CEO] wa Mfuko wa Utamaduni na Sanaa, Nyakaho Mahemba akitoa taarifa ya mfuko huo kwenye kikao hicho.

Wasanii wa Mkoa wa Mbeya wakiwa kwenye kikao hicho
Wasanii wa Mkoa wa Mbeya wakiwa kwenye kikao hicho
Wasanii wa Mkoa wa Mbeya wakiwa kwenye kikao hicho
Picha ya pamoja.

Picha ya pamoja

Share To:

dotto mwaibale

Post A Comment: