Denis Chambi, Tanga.
CHAMA cha
ACT Wazalendo jimbo la Tanga kimesema kuwa changamoto zinazowakumba
wafanyabiashara hapa nchini zisimalizwe kisiasa bali itafutiwe mbinu
mbadala wa kuondoa vikwazo wananvyokabiliana navyo ikiwemo kuundwa kwa
tume maalum itakayotoa bei elekezi ili kuondokana na adha mbalimbali
zinazoweza kujitokeza.
Wakisisitiza
kauli hiyo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika soko la
Ngamiani ,vigogo wa chama hicho Thobias Haule ambaye ni mwenyekiti wa
wilaya ya Tanga na mjumbe wa ngazi za juu na ni diwani wa kata ya
Mayomboni wilayani Mkinga Musa Jangwa walisema kuwa zipo changamoto
nyingi zinazowakumba wafanyabiashara ambazo zisipopatiwa ufumbuzi wa
haraka zinaweza kupelekea mfumuko wa bei ukazidi kuwaumiza wananchi wa
hali ya chini .
Mwenyekiti
wa chama hicho Thobias Haule alisema kuwa kuna hoja mbalimbali juu ya
madhira yanayowakumba wafanyabiashara hapa nchini huku changamoto
zikionekana kufanana zinapaswa zitatuliwe haraka ili kurahisisha
wananchi kupata bidhaa kwa gharama nafuu na kupunguza mfumuko wa bei za
bidhaa ukiwemo za chakula .
"Changamoto
zinajulikana na zipo kwenye mfumo , changamoto za wafanyabiashara
zinalingana kila sehemu , wananchi tuamke tudai haki zetu ,tusipo amka
kusimamia haki zetu hakuna atakayetusaidia " alisisitiza Haule
Kauli
hiyo imekuja kufuatia mgomo wa wafanyabiashara ulioibuka hivi karibuni
jijini Dar es salaam katika soko la kimataifa la Kariakoo ambapo mara
baada ya Waziri mkuu Kassim Majaliwa kuzungumza na wafanyabiashara hao
aliunda tume maalum itakayopitia changamoto mbalimbali zinazowakabili
ili ziweze kupatiwa ufumbuzi.
Haule
alisema bado zipo changamoto mbalimbali zinazowakabili wafanyabiashara
hasa wa hali ya chini ikiwemo mazingira duni licha ya kuwajibika kulipa
kodi hali ambayo inayosababisha mzoroto wa kiuchumi huku ubambikizaji
wa kesi kwa wananchi ukiwa nao ni kero akiiomba serikali kuzitazama kwa
ukaribu.
"Kuna
ubambikizaji mkubwa wa kesi hii nayo iangaliwe upya na ifanyiwe kazi
haraka , wananchi wanahitaji huduma bora ya maisha ikiwamo bidhaa za
vyakula kuwa chini wengi wa wafanyabiashara wakiwemo wamachinga
wanafanya shughuli zao katika mazingira magumu na yanawanyima haki yao
wakati huo huo wakiwa wanalipa kodi tunaitaka serikali iwatazame sana
wafanyabiashara hawa na kuwawekea mazingira mazuri. " alisisitiza Haule
Aidha
alihoji mkoa wa Tanga kufungwa viwanda huku baadhi ya viwanda
vikihamisha mitambo kuperekwa nje ya mkoa huo hali ambayo inazidi
kuchangia kushuka kiuchumi na kuikosesha serikali mapato.,
"Tanga
ilikuwa ni kimbilio la ajira nchini ,kila mmoja alikuwa anakimbilia
Tanga kupata ajira katika viwanda mbalimbali vilivyokuwepo wakati ule
lakini leo hii yamebakia magofu tu ,tunaomba waliopo kwenye madaraka
watuambie na watuletee majibu ya maswali ya wakazi wa Tanga kuhusu
viwanda" alihoji Haule
Diwani wa kata ya Mayomboni wilayani Mkinga Mussa Jangwa akizungumza katika mkutano wa hadhara wa chama hicho uliofanyika soko la Ngamiani jijini Tanga.
Aliyekuwa mgombea wa ubunge kwa tiketi ya chama cha ACT
Wazalendo jimbo la Korogwe mjini mwaka 2020 Bahati Chirwa, akizungumza
na wananchama wa chama hicho katika mkutano wa hadhara uliofanyika
jijini Tanga May 23, 2023.
Post A Comment: