Mkuu wa wilaya ya Nachingwea Mohamed Hassan Moyo akimpatia matone ya chanjo mmoja ya watoto waliofika katika hospital ya wilaya ya Nachingwea kuwapeleka Watoto wao kupata chanjo.

Na Fredy Mgunda, Nachingwea.

MKUU wa wilaya ya Nachingwea Mohamed Hassan Moyo amezindua wiki ya chanjo kwa Watoto wenye umri chini ya miaka mitano na wasichana wenye umri wa miaka 14 kupata chanjo ya kuzuia saratani ya mlango wa kizazi.

Akizungumza wakati uzinduzi wa wiki ya chanjo, Moyo alisema kuwa wilaya ya Nachingwea wanatarajia kuwafikia walengwa wa chanjo wapatao 1871 kwa lengo la kuwakiga na magonjwa mbalimbali.

Moyo alisema kuwa serikali ya wilaya ya Nachingwea imejipanga vikivyo kuhakikisha walengwa wote wanaotakiwa kupata chanjo wanapata katika maeneo husika ili kufanikisha kuwakinga Watoto na magonjwa mbalimbali.

Aliwaomba wazazi wote wilaya ya Nachingwea kuwapeleka Watoto wao kupata chanjo Kwenye vituo vya afya, zahanati na hospital yoyote iliyopo karibu yao.

Moyo alisema kuwa mtoto asiyepata chanjo ni hatari kwa maisha yake na kwa jamii inayomzunguka kwa kuwa atakuwa na uwezo wa kuwaambukiza wengine ugonjwa alionaa kwasababu hana kinga za kutosha kuulinda ugonjwa huo.

Alisema kuwa ni jukumu la kila mzazi kuhakikisha anamlinda mtoto wake kwa kumpeleka Kwenye vituo vya afya, zahanati na hospital yoyote ile mtoto wake akapate chanjo ya Kinga.
Share To:

mwangaza wa hbari

Post A Comment: