Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD), Mavere Tukai
 

Na Dotto Mwaibale, Babati

BOHARI ya Dawa (MSD) imeandaa Semina maalum kwa Wahariri wa vyombo vya habari nchini itakayofanyika kwa siku mbili mkoani Dodoma.

Katika taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Mavere Tukai imeeleza kuwa semina hiyo itaanza kesho Aprili 5, 2023 na kufikia tamati kesho kutwa Aprili 6, 2023 na kuwa itafanyika katika Ukumbi wa Tume ya Uchaguzi  mkoani humo.

"Lengo la semina hii ni kuwajengea uelewa kuhusu majukumu ya MSD ambayo ni manne ya kuzalisha, kununua, kutunza na kusambaza bidhaa za afya nchini sambamba na maboresho mbalimbali yanayofanywa na taasisi hiyo kupitia mpangomkakati wake wa muda mfupi na mrefu" alisema Tukai.

Tukai alisema mbali na kuwajengea uelewa Wahariri juu ya majukumu na maboresho ya MSD, semina hiyo pia itatoa fursa kwa MSD kutoa ufafanuzi juu ya masuala kadhaa ambayo yamekuwa yakijitokeza kwenye jamii, kufanya ziara naokwenye maghala ya MSD kuangalia mfumo mzima wa mnyororo wa ugavi unavyofanya kazi na kisha kutembelea baadhi ya wateja wa MSD.

Share To:

dotto mwaibale

Post A Comment: