Wanajeshi (WAJEDA) Wanandoa Valentino John Tuka na Tusibwene Mustafa Juma kutoka Songea mkoani Ruvuma wakionesha tabasamu baada ya kuachana na ukapera kwa kufunga ndoa Takatifu katika Kanisa la Moravian Usharika wa Kimara  mwishoni mwa wiki Desemba 10, 2022 jijini Dar es Salaam.
Mchungaji wa Kanisa hilo Usharika wa Kimara, Alamu Mwambande Kajuni akifunga ndoa hiyo.
Mchungaji wa Kanisa la Moravian Usharika wa Pugu Kajiungeni , Laiton Silumbwe akiongoza ibada ya ndoa hiyo Takatifu.
Wanandoa hao wakionesha furaha yao baada ya kuingia ukumbuni.
Brigedia Mstaafu, Cosmas Kayombo na mke wake walikuwa ni miongoni mwa wageni waalikwa walihudhuria hafla ya ndoa hiyo.
Ibada ya ndoa ikiendelea.
Mama Mzazi wa Bibi Harusi Ambwene Anyitike Kyoga (kulia) akionesha umahiri wa kuongoza Kwaya ya Kanisa hilo Usharika wa Pugu Kajiungeni wakati ikitoa burudani.
Baba Mzazi wa Bwana Harusi Mzee John Ambros Tuka (kushoto) akiwa kwenye ibada hiyo ya ndoa.
Ibada ikiendelea hao ni ndugu wa Bibi Harusi wakiwa kwenye ibada hiyo.
Kwaya ya kanisa hilo Usharika wa Kimara ikitoa burudani.
Kwaya ya kanisa hilo kutoka Pugu Kajiungeni ikitoa burudani.
Ibada ikiendelea.
Vijana walioshiba kisawasawa ndugu wa Bibi Harusi kutoka Pugu Kajiungeni wakiongozwa na Chambuso Alphan Shukuru  (kushoto) wakiwa kwenye hafla hiyo.
Bibi wa Bwana Harusi akitoa neno la kuwahusia wanandoa hao.
Mama mkubwa wa Bibi Harusi Mary Anyitike akitoa neno la shukurani kwa uongozi wa kanisa hilo.
Kwaya kutoka Pugu Kajiungeni ikitoa burudani.
Picha ya pamoja baada ya ibada hiyo ya ndoa Takatifu.

Dada wa Bibi Harusi Anna Segere Mirambo akiwa katika picha ya pamoja na Bibi Harusi, Tusibwene Mustafa Juma.

Picha ya pamoja Bibi Harusi na wadogo zake na dada yake Mbumi Donald Mwaibale (kulia)

Wanandoa wakiwa katika picha ya pamoja na mama zake Bibi Harusi  na Mjomba wao Donald Mwaibale (kulia)
Wanandoa wakiwa katika picha ya pamoja na wazazi wao wa pande zote mbili.
Wanandoa hao wakiwa katika picha ya pamoja na wazazi wa Bwana Harusi.
Wanandoa hao wakiwa katika picha ya pamoja na wazazi wa Bibi Harusi.
Picha ya pamoja.
Wajomba wa Bibi Harusi na mama zake wakiwa katika picha ya pamoja.
Baba wa Wanandoa hao wakiserebuka wakati wakiingia ukumbini.Kushoto ni Baba wa Bwana Harusi, John  Ambros Tuka na kulia ni Baba wa Bibi Harusi, Mustafa Juma.
Mama wa Wanandoa hao wakionesha umahiri wa kuserebuka wakati wakiingia ukumbuni. Kushoto ni Mama ya Bibi Harusi, Ambwene Kyoga na kulia ni Mama wa Bwana Harusi, Augusta Francis Mapunda.
Burudani zikiendelea kutolewa ukumbini.
Maharusi wakiwa katika picha ya pamoja na kamati yao ya maandalizi ya sherehe hiyo.
 

Na Dotto Mwaibale, Dar es Salaam

WANAJESHI (WAJEDA) Valentino John Ambros Tuka na Tusibwene Mustafa Juma kutoka Songea mkoani Ruvuma wameamua kuukimbia ukapera kwa kufunga ndoa Takatifu katika Kanisa la Moravian Usharika wa Kimara  jijini Dar es Salaam.

Ndoa hiyo iliyokuwa ya kuvutia na ya aina yake ambayo imefungwa Desemba 10, 2022 na kuhudhuriwa  na mamia ya watu ilikuwa na mvuto kutokana na shamrashara mbalimbali na burudani za kwaya mbili zilizokuwa zikitoa burudani ikiwepo kwaya ya kanisa hilo kutoka Pugu Kajiungeni na Kimara huku ikisindizwa na ngoma ya ya asili ya kabila la Wangoni.

Ndoa hiyo iliwahusisha ndugu jamaa na marafiki wa pande zote mbili wakiongozwa na wazazi wa wanandoa hao, Mzee John Ambros Tuka na mke wake Augusta Francis Mapunda wakiwa ni  wazazi wa bwana harusi na wazazi wa Bibi Harusi Mustafa Juma akiwa na mzazi mwenzake Ambwene Anyitike Kyoga.

Mchungaji wa Kanisa la Moravian Usharika wa Pugu Kajiungeni , Laiton Silumbwe akitoa wosia kwa wanandoa hao aliwaambia kuwa sasa wamekuwa mwili mmoja hivyo ndoa yao na iheshimiwe na watu  wote na silaha kubwa kwao ni kumtanguliza Mungu katika maisha yao,kudumisha upendo na kuomba msamaha pale watakapokoseana na si vinginevyo.

Alisema ndoa ni kusikilizana na haihitaji ubabe ni kila mmoja kumsikiliza mwenzake na kuwa na watoto ni majaliwa ya Mungu ambapo aliendelea kuwasisitiza wanandoa hao kumtumikia Mungu wakati wote wa maisha yao.

"Kutokana na kuwepo kwa utandawazi kumekuwa na changamoto nyingi kwenye ndoa nahata kufikia kupigana kwa wanandoa mambo haya nendeni mukayashinde kwani hayampendezi Mungu" alisema.

Mwinjiristi Atupele Kyomo kutoka kanisa hilo Usharika wa Msamala  mkoani Ruvuma ambaye aliwasindikiza wanandoa hao alisema sasa wamekuwa mwili mmoja hivyo watu wa nje wakiwepo ndugu, jamaa na marafiki waache kuwaingilia na mtu yeyote atakayehitaji msaada kwa wanandoa hao wanapaswa kuwahusisha wote.

"Kabla ya kufunga ndoa kuna baadhi ya ndugu walikuwa wakimpigia Bwana harusi au Bibi harusi wakiomba hela au mahitaji fulani lakini sasa nawaomba mambo hayo yaacheni ukiwa na shida washirikisheni wote" alisema Mwinjilisti huyo.

Ndoa hiyo ilifungwa na Mchungaji wa Kanisa hilo Usharika wa Kimara, Alamu Mwambande Kajuni  na baada ya hapo walifanya mapumiko mafupi Hoteli ya Temboni Garden ambapo wanandoa hao, ndugu,jamaa  na marafiki waliweza kupiga picha na kufuatia sherehe ya kukata na shoka ambayo iliambatana na kula na vinywaji iliyofanyika Ukumbi wa Kanisa la Romani Katoliki Parokia ya Ubungo Msewe.

Share To:

dottomwaibale

Post A Comment: