Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Iramba,Bw. Michael Matomora akimkaribisha Meneja Uhusiano na Masoko (TBS), Bi. Gladness Kaseka kwa ajili ya kutoa elimu kwa umma wilayani Iramba pamoja na kupokea zawadi ya kava za tairi kwa ajili ya kutangaza shughuli za TBS. Pia Bw. Matomora alishauri TBS kuendelea kuweka nguvu kwenye ukaguzi wa kushtukiza sokoni katika ngazi ya wilaya na vijiji.

Mkaguzi (TBS) Bw Magesa Mwizarubi akitoa elimu ya viwango kwa wananchi na wajasiriamali wilayani Iramba sambamba na kuwakumbusha namna ya kutuma maoni/malalamiko pale wanapokutana na changamoto wakati wa uzalishaji na manunuzi.
Share To:

emmanuel mbatilo

Post A Comment: