Wanamuziki wakitumbuiza katika kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Muziki Duniani yaliyofanyika wilayani Karatu mkoani Arusha Oktoba 1, 2022..
Wasanii wa kikundi cha Ngoma  cha Mahahaha wilayani Karatu wakitoa burudani wakati wa maadhimisho hayo.

Mlezi wa maadhimisho haya hapa nchini, Toriano Salamba

Katibu Mkuu wa TAMUFO, Stella Joel. 
Mlezi wa TAMUFO, Dk.Frank Richard akizungumza wakati wa maadhimisho hayo.
Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye maadhimisho hayo.

Na Dotto Mwaibale, Arusha. 

UMOJA wa Wanamuziki Tanzania (TAMUFO) umepongezwa kwa kuandaa kwa mara ya pili Siku ya  Muziki Duniani (International Music Day 2022) hapa nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari Katibu Mkuu wa TAMUFO, Stellah Joel alisema wamepokea pongezi nyingi kutoka kwa wadau wa muziki kuhusu maandalizi na maadhimisho ya siku hiyo.

Alisem maadhimisho ya siku hiyo yanafanyika kila mwaka ambapo wanamuziki hapa nchini wanaungana na wenzao duniani kote kufurahia siku hiyo.

Alisem  maadhimisho hayo  yalianzishwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) miaka mingi iliyopita lakini kwa Tanzania TAMUFO ndio waanzilishi na kuwa lengo lao likiwa ni kupanua wigo kwa wanamuziki hapa nchini  kuweza kuungana na wenzao  kimataifa na kuinua hadhi ya muziki duniani na Tanzania kwa ujumla.

Alisem maadhimisho hayo kila mwaka hufanyika Oktoba 1 na kuwa hapa nchini yalianzishwa tangu mwaka 2021 na kitaifa yanafanyika jijini Arusha ambayo mwaka huu yalifanyika katika Uwanja wa Makumbusho ya Elimu Viumbe kuanzia Septemba 28  hadi kilele chake kilifanyika Oktoba 1, 2022, wilayani Karatu na kuhusisha wanamuziki wa kada zote.

Akizungumzia kwa nini maadhimisho hayo yanafanyika Arusha alisema sababu Arusha inaanza na herufi  A na ni katikati ya Afrika na hata harakati nyingi za kudai uhuru zilifanyika Arusha na ndio maana na wao wakaona wafanyie hapo lakini.baadae wataweza kuadhimisha katika mikoa mingine.

Mlezi wa TAMUFO na mmoja aa waanzilishi wa Dk. Frank Richard alisema wataendelea kuadhimisha siku hiyo kila  mwaka na akawaomba wadau wamaendeleo kutoa ushirikiano katika kuunga mkono juhudi hizi ili kuleta Maendeleo katika Tasnia ya Muziki  kwa ujumla

Dk. Richard aliishukuru Serikali, viongozi  wa Mkoa,  Wilaya,  Taasisi, Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Cosota na Makumbusho ya Taifa kwa ushirikiano waliutoa na kuhakikisha maadhimisho hayo yanafanyinka vizuri huku pia akilishuru jeshi la polisi.

Mlezi wa maadhimisho haya hapa nchini, Toriano Salamba alisema watafanya maboresho makubwa katika maadhimisho haya kuhakikisha yanakuwa katika ubora wa kimataifa. 

Share To:

dottomwaibale

Post A Comment: