RAIS wa Jamhuri ya Kenya Willima Ruto amesema wanawashukuru watanzania wote kwa namna ambavyo waliwaombea wakati wa Uchaguzi Mkuu wa nchi yao na hivyo uchaguzi umefanyika kwa amani na wenye demokrasia.


Ruto ameyasema hayo leo Oktoba 10,2022 katika Ikulu ya Dar es Salaam wakati akizungumza mbele ya Rais Samia , maofisa wa nchi za Tanzania na Kenya pamoja na waandishi wa habari ambapo pamoja na mambo mengine ametumia nafasi hiyo kutoa shukrani kwa Watanzania kwa kuwaombea na hatimate wamefanya uchaguzi wa demokrsia.

“Tunawashukuru sana Watanzania kwa kutuombea kutujali, na kuonesha upendo wenu mkubwa kwetu wakati wote wa uchaguzi wetu kule Kenya,tunafahamu mlituombea na mliunga nasi, tunashukuru sana.Uchaguzi wetu umefanyika kwa amani na utulivu , tulikuwa na dekrasia na uchaguzi uliwazi, tunawashukuru,’amesema Rais Ruto na kuongeza “Ahsanteni sana kwa kutuombea ili tuwe na uchaguzi wa demokrasia, uchaguzi wa amani.

Awali Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kabla ya kumkaribisha Rais Ruto kuzungumza na waandishi wa habari, ametumia nafasi hiyo kuelezea amemshukuru Rais Ruto kwa kukubali kuitikia wito na kuja, hivyo amemkaribisha nchini.

“”Nipende kutumia nafasi hii kuwapongeza wananchi wa Kenya kwa kuendesha chaguzi za wazi, huru na utulivu , aidha kumpongeza tena Rais Ruto kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Kenya na nikutakie kila lakheri katika majukumu yako ya kuongoza nchi ya Kenya,”amesema Rais Samia.

Kuhusu ziara ya Rais Ruto nchini Tanzania, Rais Samia amesema ni fursa nyingine adhimu na muhimu sana kwao kama viongozi wakuu wa nchi zote mbili kwani inawawezesha kukaa pamoja kama majirani na ndugu wa damu kujadili mambo mbalimbali yanayohusu mustakabali wa maendeleo na ustawi wa mataifa yao.“Pia ni fursa inayotuwezesha kutathimini masuala mbalimbali ya uhusino wetu katika ngazi zote.”


Rais wa Jamhuri ya Kenya Mhe. Dkt. William Samoei Ruto akizungumza mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan (pichani kulia),Wageni waalikwa pamoja na Vyombo vya habari, leo Oktoba 10,2022 Ikulu jijini Dar es Salaam.
 
Share To:

Post A Comment: