Na Imma Msumba ; Arusha 

Uongozi wa Chama Cha Wamiliki wa Makampuni ya Ulinzi Tanzania Security Industry Association{TSIA} kutoka Makao Makuu kesho septemba 15 mwaka huu watakuwa na Mkutano na Wamiliki wa Makampuni ya Ulinzi Mkoani Arusha Mkutano unaotarajiwa kufanyika katika ukumbi wa Polisi Mess majira ya saa 3 asubuhi.

 Mgeni rasmi katika Mkutano huo anatarajiwa kuwa Kamanda wa polisi Mkoani Arusha,Kamishina Msaidizi wa Jeshi la Polisi Nchini,Justine Masejo na mada mbalimbali zitajadiliwa katika Mkutano huo ikiwa ni pamoja na changamoto wanazokutana nazo wamiliki wa Kampuni za Ulinzi.

 Mada nyingine ni kupanga mpango kazi wa namna ya kufanya operesheni ya ulinzi shirikishi kati ya kampuni hizo na jeshi la Polisi ikiwa na lengo la kuthibiti vitendo vya kihalifu na kufanya kazi hiyo kwa weledi mkubwa.

 Hayo yalisemwa na Mwenyekiti wa TSIA Mkoa wa Arusha James Rugangila alipokuwa akiongea na vyombo vya habari Jijini Arusha na kusema kuwa chama hicho ni walinzi shiriki katika kulinda Nchi hivyo ni wajibu wao kukutana na Polisi ili kupanga mpango kazi wa kulinda raia na mali zao.



Share To:

Post A Comment: