Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu akisalimiana na wanachama wa Saccos ya Kizimkazi Mkunguni Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar wakiongozwa na Mwenyekiti wa Saccos hiyo Bw Said Hamad Ramadhan (wa pili kushoto) wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa jengo la ofisi za Saccos hiyo iliyoambatana na upokeaji wa samani mbalimbali kutoka Benki ya NBC kwa ajili ya saccos hiyo. Wengine ni pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Bw Theobald Sabi. Hafla hiyo ilifanyika mwishoni mwa wiki visiwani Zanzibar


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu (katikati) akijipongeza na baadhi ya viongozi serikali, chama na benki ya NBC mara baada ya kukata utepe kuashiria uzinduzi wa ofisi za Saccos ya Kizimkazi Mkunguni Mkoa wa Kusini Unguja wakati wa hafla fupi iliyoambatana upokeaji wa samani mbalimbali zilizotolewa na Benki ya NBC kwa ajili ya saccos hiyo. Pamoja nae ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Katiba Sheria, Utumishi na Utawala Bora wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Haroun Ali Suleiman (Kulia), Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Rashid Hadid Rashid ( wa pili kulia), Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Bw Theobald Sabi (wa tatu kushoto) na Mratibu wa Saccos hiyo Bw Said Ramadhani Mgeni (wa pili kushoto)


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu (wa tatu kushoto) akijipongeza na baadhi ya viongozi serikali, chama na benki ya NBC mara baada ya kuzindua ofisi ya Saccos ya Kizimkazi Mkunguni Mkoa wa Kusini Unguja wakati wa hafla fupi iliyoambatana upokeaji wa samani mbalimbali zilizotolewa na Benki ya NBC kwa ajili ya saccos hiyo. Pamoja nae ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Katiba Sheria, Utumishi na Utawala Bora wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Haroun Ali Suleiman (wa pili kushoto), Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Rashid Hadid Rashid ( kulia) na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Bw Theobald Sabi (wa pili kulia).


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu (alieketi) akimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Bw Theobald Sabi akifafanua kuhusu mchango wa benki hiyo katika kuunga mkono jitihada za serikali katika kujenga mfumo jumuishi wa fedha (Financial Inclusion) na kusogeza huduma karibu zaidi na wananchi wakati wakati hafla fupi ya uzinduzi wa ofisi ya Saccos ya Kizimkazi Mkunguni Mkoa wa Kusini Unguja iliyoambatana upokeaji wa samani mbalimbali zilizotolewa na Benki ya NBC kwa kwa ajili ya saccos hiyo mwishoni mwa wiki.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu (Katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi waandamizi wa benki ya NBC wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo Bw Theobald Sabi wakati hafla fupi ya uzinduzi wa ofisi ya Saccos ya Kizimkazi Mkunguni Mkoa wa Kusini Unguja iliyoambatana upokeaji wa samani mbalimbali zilizotolewa na Benki ya NBC kwa kwa ajili ya saccos hiyo mwishoni mwa wiki.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu akizungumza na wakazi wa Kizimkazi Mkunguni Mkoa wa Kusini Unguja wakati hafla fupi ya uzinduzi wa ofisi ya Saccos ya Kizimkazi Mkunguni iliyoambatana upokeaji wa samani mbalimbali zilizotolewa na Benki ya NBC kwa kwa ajili ya saccos hiyo mwishoni mwa wiki.




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu akisalimiana na baadhi ya maofisa waandamizi wa benki ya NBC wakati hafla fupi ya uzinduzi wa ofisi ya Saccos ya Kizimkazi Mkunguni Mkoa wa Kusini Unguja iliyoambatana upokeaji wa samani mbalimbali zilizotolewa na Benki ya NBC kwa kwa ajili ya saccos hiyo mwishoni mwa wiki.


Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo Bw Theobald Sabi (katikati walioketi) akiwa kwenye picha ya pamoja na wanachama wa Saccos ya Kizimkazi Mkunguni Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar wakiongozwa na Mwenyekiti wa Saccos hiyo Bw Said Hamad Ramadhan (wa pili kushoto walioketi) wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa ofisi za Saccos hiyo iliyofanyika mwishoni mwa wiki ikiambatana na upokeaji wa samani mbalimbali kwa ajili ya saccos hiyo zilizotolewa na Benki ya NBC mwishoni mwa wiki.

Na Mwandishi Wetu-Zanzibar

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu amezipongeza taasisi za fedha nchini ikiwemo benki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa namna zinavyoendelea kuunga mkono juhudi za Serikali katika kujenga mfumo jumuishi wa fedha (Financial Inclusion) huku akionesha kuguswa na jitihada za taasisi hizo katika uwezeshaji wa jamii kiuchumi hususani makundi ya wanawake na vijana.

Akizungumza wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa jengo la ofisi ya Saccos ya Kizimkazi Mkunguni Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar iliyoenda sambamba na upokeaji wa samani mbalimbali zilizotolewa na Benki ya NBC kwa ajili ya saccos hiyo, Rais Samia alionesha kuguswa na namna taasisi za kifedha zilivyo mstari wa mbele katika kuchochea uchumi jumuishi huku pia zikitumia vema sehemu ya mapato yao kurejesha kwa jamii kupitia misaada mbalimbali inayoendelea kutolewa na taasisi hizo.

“Naamini kupitia Saccoss hii ya Kizimkazi wananchi wengi wa eneo hili watafikiwa na huduma muhimu za kifedha na hivyo kuleta ukombozi wa kiuchumi kwa kaya nyingi za eneo hili. Nitoe shukrani zangu za dhati kabisa kwa Benki ya NBC kwa namna ilivyoguswa na jitihada za wakazi hawa wa Kizimkazi na hivyo kuamua kuwaunga mkono kwa kuwapatia msaada wa samani za ndani ikiwemo viti na meza kwa ajili ya ofisi yao…hongereni sana benki ya NBC,’’ alisema Rais Samia.

Rais Samia alitoa wito kwa wananchi kutumia vema ushirikiano unaotolewa na taasisi hizo katika nyanja mbalimbali ikiwemo elimu, afya, michezo na kiuchumi ili waweze kujikwamua kiuchumi na kijamii kwa kuhakikisha wanaitumia vema misaada hiyo ili iweze kuwanufaisha wananchi wengi na kwa muda mrefu zaidi.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Bw Theobald Sabi alisema msaada huo ni mwendelezo wa jitihada za benki hiyo katika kuunga mkono jitihada za serikali katika kujenga mfumo jumuishi wa fedha (Financial Inclusion) na kusogeza huduma karibu zaidi na wananchi.

“Kupitia Saccoss hii wananchi wengi wanakwenda kufikiwa na huduma za kifedha wakiwemo vijana, wazee na kina mama hatua ambayo itawawezesha kupata mikopo kwa ajili ya kukuza mitaji yao ya kibiashara na kujiongezea kipato kwa faida ya uchumi wao na familia zao. Benki ya NBC tumekuwa mstari wa mbele kuunga mkono kila jitihada zinazofanywa na wananchi kibiashara na kiuchumi kwa kuwa tuna malengo yanayofanana,’’ alibainisha.

Alisema si mara ya kwanza kwa benki hiyo kushirikiana na wakazi wa Kizimkazi katika miradi ya maendeleo huku akitolea mfano wa ujenzi wa madarasa kwa ajiili ya shule ya awali ya Kizimkazi-Mkunguni ulioambatana na utoaji wa msaada wa gari maalum la tiba yaani (Mobile Clinics) inayotoa bure huduma kwa ajili ya Mama na Mtoto kwa maeneo mbalimbali visiwani Zanzibar.

“Misaada yote imekuwa matokeo chanya kwa jamii hii na sisi kama Benki na mdau wa maendeleo, tunajivunia sana kuwa sehemu ya suluhu ya changamoto za jamii yetu.’’ Alisema

Awali akitoa taarifa fupi kuhusu Saccos hiyo, Mratibu wa Saccos ya Kimzikazi Bw Said Ramadhani Mgeni alisema licha ya ujenzi wa jengo hilo kuanza mwaka 2015 ulikwama kuendelea kutokana na kukosekana kwa fedha hadi pale Rais Samia ambae pia ni Mwanachama wa Saccos hiyo aliposaidia juhudi hizo kwa kuchangia fedha kiasi cha sh milioni 55 iliyosaidia kukamilisha mradi huo.

“Kukamilika kwa mradi huu kunatoa fursa kwa wananchama na wakazi wa vijiji jirani kuihifadhi fedha karibu kabisa na makazi yao huku pia ujenzi wa ofisi hiyo ukitarajiwa kutoa huduma ya ukumbi kwa wakazi kizimkazi pindi tutakapokuwa na mikutano yetu na kwenye hili tunawashukuru sana Benki ya NBC kwa msaada wao wa samani za ndani ikiwemo viti na meza ambavyo tunaahidi kuvitunza na kuvilinda’’ alisema.
Share To:

emmanuel mbatilo

Post A Comment: