Mkuu wa mkoa wa singida Mhe. Peter Serukamba ameridhishwa na jinsi wilaya ya ikungi inayoendesha zoezi la sensa ya watu na makazi kwa mwaka 2022 na kuitaka wilaya leo jumamosi tarehe 27/08/2022 wamalize zoezi lote la sensa ya watu na makazi 


Rc Serukamba amesema kama mpaka sasa wilaya imeshafikisha zaidi ya asilimia 85 kwa kuandikisha kaya zaidi ya elfu 51 kuna uwezokano mkubwa wakamaliza zoezi hilo mapema iwezekanavyo


Wakati huo huo Rc Serukamba amewataka wasimamizi na waratibu wa sensa ikungi kuwahamisha makarani waliomaliza katika maeneo yao na kuwapeleka kwenda kuongeza nguvu katika maeneo ambayo hayajafikiwa na yana idadi kubwa ya kaya uku zingine zikiwa kwenye umbali kufikiwa 


Mkurugenzi wa halmashauri ya Ikungi Ndugu Justice Kijazi amemuhakikishia Rc Serukamba kuwa zoezi litakwenda vizuri na litamalizika katika muda uliopangwa na kwa uadilifu mkubwa 



Share To:

Post A Comment: